2021
Wamisionari Walihubiri Injili
Aprili 2021


“Wamisionari Walihubiri Injili,” Rafiki, Aprili 2021

Ujumbe wa kila mwezi wa gazeti la Rafiki, Aprili 2021

Wamisionari Walihubiri Injili

Picha
wamisionari wawili wa karne ya 19

Vielelezo na Apryl Stott

Baada ya Kitabu cha Mormoni kupigwa chapa, Mungu aliwaita wamisionari waende kuwafundisha watu zaidi kuhusu kitabu hicho.

Picha
Samuel Smith akipanga nakala za Kitabu cha Mormoni

Kaka wa Joseph Smith, Samuel, alibeba begi lililojaa nakala za Kitabu cha Mormoni kwa ajili ya kuzigawa. Watu walikusanyika ili kumsikiliza akifundisha.

Picha
mmisionari wa karne ya 19 akifundisha katika visiwa vya Pasifiki

Wamisionari wengine walifundisha watu huko Ulaya. Wengine walifundisha watu waliokuwa wakiishi katika visiwa.

Picha
dada mmisionari wa karne ya 19 huko Uingereza.

Baadaye, akina dada wamisionari rasmi wa kwanza waliitwa kuhudumu huko Uingereza.

Picha
watoto wakiwa katika uwanja wa michezo, wakisoma Kitabu cha Mormoni

Ninaweza kuwa mmisionari pia. Ninaweza kushiriki Kitabu cha Mormoni na wengine.

Ukurasa wa Kupaka Rangi

Ninaweza kufundisha injili

Picha
watoto wakiwa na picha za Yesu

Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwaelezea wengine kuhusu Yesu Kristo?

Chapisha