2022
Mwokozi Anayeteseka
Aprili 2022


“Mwokozi Anayeteseka,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Aprili 2022.

Ujumbe wa kila Mwezi wa Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Aprili 2022

Mwokozi Anayeteseka

Mamia ya miaka kabla ya Yesu Kristo kuja, Isaya alitoa unabii wa kuteseka kwake kwa ajili ya dhambi zetu.

kudharauliwa na kukataliwa

Picha
Mikono ya Yesu Kristo imefungwa

Wakati Yesu Kristo alipokuja duniani, watu wengine walimwamini, lakini wengi hawakumwamini. Hata walimdharau na wengi wakamchukia. Mwishowe, watu waliamua ateswe na kuuawa. (Ona 1 Nefi 19:9.)

amezibeba huzuni zetu

Picha
Yesu Kristo akiomba katika Gethsemane

Yesu Kristo alibeba maumivu, ugonjwa na unyonge wetu wote. Alifanya haya ili atuhurumie na kujua jinsi ya kutusaidia. (Ona Alma 7:11–13.)

aliumia kwa ajili ya makosa yetu

Picha
Yesu Kristo msalabani

Yesu Kristo aliteseka kwa ajili ya dhambi zetu. Alifanya haya ili tusamehewe tunapotubu. (Ona Mafundisho na Maagano 18:11; 19:15–19.)

na kwa mapigo yake tunaponywa

Picha
watu wakihisi mkono wa Yesu Kristo aliyefufuka

“Mapigo yake” ni vidonda Vyake. Haya yanasimamia mateso yote aliyovumilia kwa ajili yetu, ikiwemo kumwaga damu na kifo chake. Kwa sababu Yesu Kristo aliteseka kwa ajili yetu, tunaweza kufanywa upya tena. Dhabihu Yake inawezesha dhambi zetu kusamehewa. Tunapotubu na kujaribu kushika maagano yetu, anatuponya na kutubadilisha. (Ona Mosia 3:7–11; Makala ya Imani 1:3.)

Chapisha