Historia ya Kanisa
“Nilijua Kwamba Ilikuwa Kweli”


“Nilijua Kwamba Ilikuwa Kweli”

Mwanzoni mwa miaka ya 1970, Watakatifu wa Siku za Mwisho walioishi Kenya kwa muda walifanya mikutano nyumbani mwao. Idadi ndogo ya watu walijiunga na Kanisa.

Mwanzoni mwa miaka ya 1980, Gideon Kasue alikubali kazi kama mhudumu kwenye mgahawa wa Hunter Lodge, hoteli ya kitalii karibu na Kiboko (kilomita 155 [maili 96] kusini mashariki mwa Nairobi), ili kumkimu Esther, mkewe, pamoja na watoto wao tisa. Nafasi hii ya kazi ilimlazimu Gedeon kuishi na kufanya kazi kwenye Hoteli, karibu kilomita 100 (maili 62) kutoka makazi ya familia kwenye miinuko ya Kilungu. Karla na Dennis Child, Watakatifu wa Siku za Mwisho waliokuwa wakifanya kazi kwenye kituo cha utafiti kilichopo karibu walifanya urafiki na Gideon na Benson Mwanaye.

Watoto walimwalika Benson kuungana nao kwenye huduma ya kanisa la nyumbani na walimpa kipeperushi chenye simulizi juu ya Joseph Smith na nakala ya Kitabu cha Mormoni. Wakati Benson akisoma simulizi juu ya Joseph Smith, hisia ya kustaajabisha kwamba ilikuwa ni ya kweli ilimzidia na kumshawishi kufanya utafiti wake mwenyewe. Kwenye maktaba ya shule, Benson alitafuta neno “Mormon” kwenye Kamusi ya Kiingereza ya Oxford. Maana ya neno ilisisitiza juu ya ndoa za mitaala kati ya waumini wa kale katika njia ambayo ilionyesha ndoa za mitaala katika mtazamo hasi. Kwa sababu ndoa za mitaala ilikuwa jambo la kawaida Kenya, Benson hakuwa na uhakika kwa nini ilikuwa tatizo.

Wakati wa mkutano wake uliofuata na watoto, Benson aliwaonyesha maana ya neno na kuwaomba wafafanue. Wakati watoto wakifafanua historia ya Kanisa, Benson alihisi hisia sawa na zile za kustaajabisha zikithibitisha ukweli aliouhisi awali. Benson punde alishiriki na Nickson kaka yake kipeperushi kuhusu Joseph Smith. “Nilijua kwamba ilikuwa ni kweli,” Nickson alikumbuka. Benson na Nickson walianza kushiriki na familia na marafiki zao kile walichojifunza.

Wengi walitengeneza uthibitisho imara kwenye injili ya urejesho na kuanza kuomba kubatizwa. Hata hivyo, mnamo mwanzoni mwa miaka ya 1980, Kanisa lilikuwa halijasajiliwa Kenya na halingeweza kufanya ubatizo, kuanzisha matawi au kuwa na mikutano ya mara kwa mara kwenye umma.

Familia ya Kasue walitafuta ushauri wa mwanasheria mkuu wa serikali ya Kenya, ambaye pia alikuwa mmoja wa watu wa kabila lao la Wakamba. Waliambiwa kwamba hakukuwepo na sheria iliyokataza imani yao—ikijumuisha ubatizo—ilimradi umefanywa kwa siri. Kundi likawa imara, na watu wapya wakihudhuria mikutano yao binafsi kila wiki.

Picha
Gideon Kasue

Gideon Kasue (katikati) pamoja na wana wake wawili, circa 1991.

Wakati kikundi hiki kidogo kikikua, ugumu wa kukutana uliongezeka kwa sababu baadhi ya mamlaka za maeneo husika zilitafuta kusimamisha shughuli zao. Uhitaji wa kuificha imani yako kutoka macho ya umma ukawa jaribu kubwa kwa wengi wa waongofu wapya, ambao walitamani sana kushiriki injili. Washiriki waliendelea na mifungo na sala za dhati kwa ajili ya Kanisa kusajiliwa nchini. Hatimaye, baada ya zaidi ya mwongo mmoja wa maombi, Kanisa lilisajiliwa rasmi mnamo Februari 1991. Wilaya ilianzishwa Nairobi baadaye mwaka huo.

Chapisha