2017
Kuwaombea wengine
Februari 2017


Vijana

Kuombea Amani

Mwandishi anaishi Arizona, Marekani.

Wazazi wangu mara nyingi walihudhuria mikutano baada ya kanisa, nami ningewaangalia ndugu zangu wadogo watatu na kuwasaidia kuandaa chakula cha mchana—ingawaje walikuwa mara nyingi wenye kukasirika haraka na wenye njaa. Kama kawaida ikiwa wangeanza kupigana, ningeweza kutatua shida hiyo ndogo kwa haraka. Lakini mara nyingine ilikuwa vigumu kuleta amani wakati mapigano yalipoanza kwa sababu ningehamaki.

Alasiri moja, ndugu zangu walikuwa na wakati mgumu hasa wa kuvumiliana. Niligundua kwamba juhudi zangu za kuleta amani zilifanya mambo kuwa mabaya zaidi kwa sababu nilikuwa nakasirika. Hivyo basi nilitayarisha chakula changu cha mchana na kunyamaza. Hatimaye, nilitangaza, “Nitasali. Je, tunaweza kuwa kimya kwa dakika moja?” Punde tu walipotulia, nilibariki chakula. Kabla ya kufunga maombi, niliongezea, “Na tafadhali tusaidie kuwa wapatanishi.”

Mwanzoni, walionekana kutosikia na wakaanza kupigana tena. Nilikuwa nimekasirika lakini nilijua nilihitaji kuwa mwenye kupenda na mtulivu kadiri iwezekanavyo kwa sababu nilikuwa nimesali tu kuombea amani iwepo. Baada ya muda kidogo, nilijihisi kuwa mtulivu sana. Nilikula bila kusema lolote, na wavulana hatimaye waliacha kupigana. Nilitambua kwamba amani niliyohisi ilikuwa jibu la ombi langu. Nilikuwa nimesali ili niwe mpatanishi, na Baba wa Mbinguni alikuwa amenisaidia kuwa mtulivu wakati ilikuwa rahisi mno kukema. Ninajua ya kwamba hakika anaweza kutupa amani.

Chapisha