Maandiko Matakatifu
Mawazo ya Kutumia Programu ya Maktaba ya Injili


“Mawazo ya Kutumia Programu ya Maktaba ya Injili,” Mawazo ya Kujifunza Maandiko (2021)

“Mawazo ya Kutumia Programu ya Maktaba ya Injili,” Mawazo ya Kujifunza Maandiko

Picha
mwanamke na mtoto wakiangalia kwenye tableti

Mawazo ya Kutumia Programu ya Maktaba ya Injili

Sikiliza

Mojawapo wa njia bora zaidi ya kujifunza maandiko ni kusikiliza rekodi mbalimbali. Unaweza kufanya hili nyumbani kwako au popote pale. Unaweza pia kusikiliza kwa kasi tofauti na kwa lugha tofauti.

Jifunze kwa Mada

Unaweza kupata maandiko juu ya mada iliyotolewa kwa kutumia kipengele cha utafutaji na kisha kupitia matokeo yanayoshabihiana na utafutaji huo. Pia unaweza kutumia chapisho la Mada za Injili ambalo hutoa maandiko muhimu kwa ajili ya mada fulani.

Iliyopangiliwa kwa Mada

Unaweza kupanga maudhui kwa mada ukitumia “Vitambulisho” na “Madaftari ya kuandikia mambo muhimu.” Mada hizi zinaweza kuwa muhimu wakati unapotayarisha hotuba au somo.

Weka alama kwa rangi inayoangaza

Unaweza kuwekea alama maandiko yako kwa rangi inayoangaza au vitu vingine kwa kuchagua kifungu na kisha kuchagua mtindo. Mtindo unaweza kuwa mchanganyiko wa rangi tofauti na mstari au rangi ya kuangaza.

Tengeneza Viungo

Unaweza kutengeneza viungo kati ya maandiko, ujumbe wa mkutano mkuu, na maudhui mengine. Hii inaweza kukusaidia kukumbuka na kwa haraka kupata miunganiko ambayo umeitengeneza.

Angalia Ufafanuzi

Unaweza kutafuta kwa urahisi ufafanuzi wa neno katika maandiko kwa kulichagua na kubofya kitufe cha “Fafanua”

Tumia Alamisho na Skrini

Unaweza kurudi haraka kuchagua maudhui kwa kutumia alamisho ili kufuatilia maeneo na skrini zingine. Kutumia alamisho kunaweza kukuwezesha kuweka sura na maudhui anuwai wazi kwa wakati mmoja.

Weka Ratiba

Unaweza kuunda mpango wa kujifunza ambao unakusaidia kufuatilia maendeleo yako ya kujifunza maandiko. Unaweza pia kuweka vikumbusho kukusaidia kutimiza malengo yako ya kujifunza. Ratiba inaweza kukusaidia kwenda sambamba na ratiba ya Njoo, Unifuate au usomaji binafsi wa Kitabu cha Mormoni.

Chapisha