Maandiko Matakatifu
Kwa nini Ujifunze Maandiko?


Kwa nini Ujifunze Maandiko? Mawazo ya Kujifunza Maandiko (2021)

Kwa nini Ujifunze Maandiko? Mawazo ya Kujifunza Maandiko

Picha
Kristo anaanzisha sakramenti kati ya Wanefi, na Andrew Bosley

Kwa nini Ujifunze Maandiko?

Tunapojifunza maandiko kwa bidii, tunasogea karibu na Yesu Kristo na kuelewa vizuri injili Yake na dhabihu Yake ya upatanisho. Nabii Nefi alitutia moyo kwa njia hii:

“Kwa hivyo, lazima msonge mbele mkiwa na imani imara katika Kristo, mkiwa na mng’aro mkamilifu wa tumaini, na upendo kwa Mungu na wanadamu wote. Kwa hiyo, kama mtasonga mbele, mkila na kusherehekea neno la Kristo na mvumilie hadi mwisho, tazama, hivi ndivyo asema Baba: Mtapokea uzima wa milele” (2 Nefi 31:20).

Picha
familia ikisoma maandiko

Mafundisho kutoka kwenye maandiko yatatusaidia kurudi kwa Baba yetu wa Mbinguni. Manabii wetu wa siku za mwisho wametuomba tujifunze mara kwa mara kama watu binafsi na, ikiwezekana, kama familia. Wametualika tujifunze kutoka kwenye uzoefu wa wale walio katika maandiko na kutumia hadithi na mafundisho ya maandiko kwenye maisha yetu leo, kama vile Nefi anavyoshauri katika 1 Nefi 19:23. Manabii wa zamani na wa sasa wametualika kusoma maandiko na “kusherehekea maneno ya Kristo” (2 Nefi 32:3).

Picha
mwanamume akisoma maandiko

Rais Russell M. Nelson pia alifundisha ukweli huu muhimu juu ya “kusherehekea” maandiko:

“Kusherehekea inamaanisha zaidi ya kuonja. Kusherehekea inamaanisha kufurahia. Tunafurahia maandiko kwa kujifunza kwayo katika moyo wa ugunduzi mwema na utii wenye uaminifu. Wakati sisi tunaposherehekea maneno ya Kristo, yanaingia ‘katika vibao vya mioyo ya nyama.’ [2 Wakorintho 3:3]. Yanakuwa sehemu muhimu ya asili yetu” (“Kuishi Kulingana na Mwongozo wa Maandiko,” Ensign, Nov. 2000, 17).

Tunaposhiriki mara kwa mara katika kujifunza maandiko kwako binafsi na kama familia, sisi na familia zetu tunaweza kuongozwa, kulindwa, na kuimarishwa dhidi ya changamoto nyingi za siku yetu.

Chapisha