2010
Kitabu Changu cha Binafsi cha Mormoni
Septemba 2010


Vijana

Kitabu Changu cha Binafsi cha Mormoni

Mnamo Agosti 2005, Rais Gordon B. Hinckley (1910–2008) alitoa changamoto kwa washiriki wa Kanisa kusoma Kitabu cha Mormoni kabla ya mwisho wa mwaka, nilijiahidi nitasoma kitabu chote. Niliikuwa nazielewa hadithi zilizo ndani ya Kitabu cha Mormoni lakini kamwe nilikuwa sijakisoma chote. Sasa nilikuwa tayari kuweka hii ahadi yangu.

Nilikuwa nimefunzwa kutumia maandiko katika maisha yangu na kuyafanya kuwa yangu. Basi nilikuwa nikisoma, niliandika kwenye pembe ya ukurasa kile nilichofikiria kuwa wazo muhimu la aya. Pia nilipiga msitari maneno na vifungu vilivyorudiwa kuonyesha mkazo.

Niliweka jina langu karibu na majina katika maandiko ili kunisaidia kukumbuka kwamba neno la Mungu lililosemwa kwa wengine pia linaweza kusemwa kwangu. Kwa mfano, katika 2 Nefi 2:28 niliandika jina langu: Na sasa, [Hillary], ningetaka utazame yule Mpatanishi mkuu, na usikilize amri zake kuu.” Jinsi nilivyozidi kukifanya Kitabu Changu cha Binafsi cha Mormoni, ndivyo nilivyopata moyo kukisoma kila siku.

Nilivyosoma kila siku, maombi yangu yakawa ya kuhisi moyoni na ya kibinafsi. Pia nikaweza kushikilia vilazi vyangu na kufuata mwongozo wa Roho na kufanya urafiki na wengine. Katika siku ya mwisho ya mwaka, nilimaliza Kitabu cha Mormoni.

Basi nilifahamu umuhimu wa kusoma Kitabu cha Mormoni chote, pamoja na maandiko mengine, na kutaka hivyo mara nyingi sana katika maisha yangu.

Chapisha