2010
Kitabu cha Mormoni kama Mwongozo wa Kibinafsi
Septemba 2010


Ujumbe wa Urais wa Kwanza, Septemba 2010

Kitabu cha Mormoni kama Mwongozo wa Kibinafsi

Sisi sote tunaishi, katika nyakati zetu bora1, tamaa ya kurudi nyumbani kuishi na Mungu. Alitupatia kipawa cha Mwanawe Mpendwa kama Mwokozi kutoa njia na kutufunza jinsi ya kuifuata. Alitupatia manabii kuonyesha njia. Nabii Joseph Smith aliongozwa kutafsiri kumbukumbu za manabii ambayo ndio Kitabu cha Mormoni. Ndio mwongozo wetu halisi wa njia yetu ya nyumbani kwa Mungu.

Joseph Smith alisema juu ya kitabu hiki cha thamani, “Niliwaambia ndugu kwamba Kitabu cha Mormoni ndicho kitabu sahihi duniani, na ndicho jiwe la katikati la leo la dini yetu, na kuwa mwanadamu angemkaribia Mungu zaidi kwa kufuata mafunzo yake, zaidi ya kitabu kingine”1

Mafunzo ya Kitabu cha Mormoni ni amri za Mungu tunazozipata ndani yake. Kati yake ni amri moja kwa moja kutoka kwa Mwokozi kupitia kwa manabii wake juu ya kile tunachopaswa kufanya na kile tunaweza kuwa. Kitabu cha Mormoni kinatupatia mfano wa Mwokozi ili kuongeza imani yetu na azimio la kutii amri zake ili kumfuata yeye. Kitabu hiki kimejaa mafundisho ya Kristo ya kutuongoza. Hapa kuna mfano kutoka 2 Nefi:

“[Yesu] akawaambia watoto wa watu: Nifuateni mimi. Kwa hivyo, ndugu zangu wapendwa, je, tunaweza kumfuata Yesu tusipokubali kushika amri za Baba?

“Na Baba akasema: Tubuni, tubuni, na mbatizwe katika jina la Mwana wangu Mpendwa” (2 Nefi 31:10–11).

Kitabu hiki kinaonyesha wazi kwamba ni sharti tupokee Roho Mtakatifu kama ubatizo wa moto ili kutusaidia kukaa katika njia iliyosonga na nyembamba. Tunafunzwa kwamba sharti tuombe daima katika jina la Kristo, bila kusita4 na kama tutafanya hivyo, tuna ahadi hii: “Kwa hivyo, lazima msonge mbele mkiwa na imani imara katika Kristo, mkiwa na mng’aro mkamilifu wa tumaini, na upendo kwa Mungu na wanadamu wote. Kwa hivyo, kama mtasonga mbele, mkila na kusherekea neno la Kristo, na mvumilie hadi mwisho, tazama, hivi ndivyo asema Baba: Mtapokea uzima wa milele” (2 Nefi 31:20).

Kitabu cha Mormoni kinaonyesha wazi katika mahubiri ya ajabu ya Mfalme Benyamini maana ya kuwa na upendo wa Mungu na watu wote. Uasili wetu unapobadilishwa ni nguvu za Upatanisho na kupitia utiifu wa uaminifu amri, tunajazwa na upendo wa Mungu (ona Mosia 4:1–12).

Kitabu cha Mormoni pia kinatupatia imani kwamba tunaweza kuwa tumetakaswa sana katika maisha haya kwamba hatutakuwa na tamaa ya kutenda dhambi (ona Mosia 5:2). Haya matumaini yanatupatia ujasiri na faraja wakati Shetani anapotujaribu na kutuvunja moyo katika njia yetu.

Kila mara ninaposoma hata mistari michache katika Kitabu cha Mormoni, ninahisi ushuhuda wangu ukiimarika kwamba kitabu hiki ni cha kweli, kwamba Yesu ndiye Kristo, kwamba tunaweza kumfuata Yeye nyumbani, na kwamba tunaweza kuwachukua wale tunaopenda nyumbani pamoja nasi. Kimekuwa kwangu kitabu cha vitabu. Ni neno la Mungu.

Naomba kwamba sisi na wale wote tunaowapenda tutakunywa kwa kina na kila siku kutoka kwacho. Nashuhudia katika jina Yesu Kristo kwamba ni mwongozo wa kweli.

Muhtasari

  1. Teachings of Presidents of the Church: Joseph Smith (2007), 64.

Kufundisha kutoka kwa Ujumbe huu

Tunapotumia maandiko na maneno ya manabii wa siku za mwisho kama vyanzo vya mafunzo yetu yote, hualika Roho kushuhudia. Hii inaleta kwenye mafunzo yetu ‘uwezo wa Mungu hata katika kuwashawishi watu’ (M&M 11:21)” (Teaching, No Greater Call [1999], 51). Fikiria kusoma mkazo kutoka kwa Ujumbe wa Rais Eyring, pamoja na matamshi ya Joseph Smith juu ya Kitabu cha Mormoni. Alika wanafamilia kushirikisha jinsi kuishi mafunzo yanayopatikana katika Kitabu cha Mormoni kumewasaidia kusongea karibu na Mungu.

“Wanaojifunza wanapozungumza juu ya kanuni kutoka kwenye maandiko, wanakuza ujuzi wanahitaji kwa mafunzo yao ya maandiko ya kibinafsi” (Teaching, No Greater Call, 54). Fikiria juu ya kusoma maandiko yaliyotajwa katika huu ujumbe na ukitafuta na kuzungumza kanuni zinazofunzwa.

Chapisha