2013
Kusikiliza msukumo
Januari 2013


Vijana

Kusikiliza Msukumo

Usiku mmoja binamu wangu mdogo alitoroka kutoka nyumbani, kwa hivyo niliharakisha kuenda kumtafuta. Nilipokuwa nikiendesha gari, niliomba Roho aweze kunisaidia. Nilijua kwamba Mungu angeweza kujibu na kunielekeza, na nilijaribu kusikiliza msukumo wa Roho. Lakini wakati nilikosa kusikia chochote, nilianza kuwa na hofu sana na nikahisi kwamba Roho hakuwa akinipatia msukumo.

Ingawa nilikuwa nikitaka kuendelea mbele na kutafuta, nilihisi kwamba nikae katika eneo lililo karibu na nyumba ya binamu wangu. Kwa hivyo niliamua kuendesha gari katika eneo hilo mara ingine. Niliposimama katika makutano, niliona twasira ya umbo la mshichana mdogo akitembea. Nilikuwa nimempata binamu yangu!

Nilipokuwa nikitoka garini na kumkimbilia, nilitambua kwamba Roho alikuwa amenielekeza mimi wakati wote kwa kunisaidia kuhisi kwamba ninafaa kukaa katika eneo hilo hilo. Kwa sababu nimekuwa nikisikiliza sauti tulivu, karibu ningepuuza msukumo wa Roho. Kisha nikaelewa kwamba mara nyingi sisi hatutasikia sauti, bali tutahisi maonyesho katika mioyo yetu.

Nilikuwa na shukrani sana kwa maongozi ya Roho. Kwa kweli Yeye daima yupo! Kama maandiko yanavyosema, “Roho Mtakatifu atakuwa mwenzi wako daima” (M&M 121:46).

Kama sisi tutakuwa wastahiki kwa maongozi ya Roho na kuwa na usikivu, tunaweza kuwa vyombo katika mikono ya Mungu kufanya mema kwa watu wengi. Tukiwa na wenzi wa Roho daima, tutajua njia tunayopaswa kuenda.

Chapisha