2017
Furaha kama Mwanafunzi wa Yesu Kristo.
August 2017


Vijana

Furaha kama Mwanafunzi wa Yesu Kristo.

Je, umeshawahi kuwa na siku mbaya? Ulifanya nini ili kujichangamsha? Rais Uchtdorf anajua ya kwamba “sisi kila mmoja tunazo huzuni zetu, masikitiko yetu, masononeko yetu. Tunaweza kuhisi kukata tamaa na wakati mwingine kuzidiwa kabisa.”

Suluhu yake ni kusihi kile anachokiita “maisha ya mwanafunzi”: “salia mwaminifu na endelea kusonga mbele kwa imani.” Wakati tunaposonga mbele kwa imani, tunaweza kumwamini Mungu, kutii amri Zake, na kuwahudumia wengine—na kuhisi furaha wakati huo wote. Kama Rais Uchtdorf alivyosema, “Wale wanaoishi maisha ya mwanafunzi … ni wale ambao matendo yao madogo mara nyingi huleta tofauti kubwa.”

Fikiria kuandika orodha ya jinsi unavyoweza kuishi maisha ya mwanafunzi. Kwa mfano, unaweza kuandika chini wazo la kutoa huduma kama vile “Saidia mzazi kuandaa chakula cha jioni” au wazo la kutii amri kama vile “Kusali niwe na subira zaidi na ndugu zangu.” Wakati mwingine unapohisi kukata tamaa au umeshindwa kabisa, tazama orodha yako, chagua wazo moja, na ulijaribu.

Chapisha