Njoo, Unifuate
Oktoba 14–20. Wafilipi; Wakolosai: ‘Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu’


“Oktoba 14–20. Wafilipi; Wakolosai: ‘Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2019 (2019)

“Oktoba 14–20. Wafilipi; Wakolosai,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
Paulo akitoa imla ya barua toka gerezani

Oktoba 14–20

Wafilipi; Wakolosai

“Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu”

Soma Wafilipi na Wakolosai, ukifikiria kuhusu watoto unaowafundisha. Tafuta mwongozo wa kiungu kuhusu jinsi ya kuwafundisha kanuni zilizo katika nyaraka hizi .

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waulize watoto walifanya nini wiki hii iliyopita ili kumfikia mtu fulani aliyehitaji rafiki, kama ilivyojadiliwa darasani wiki iliyopita.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

Wafilipi 1:3–4; Wakolosai 1:3, 9

Viongozi wa Kanisa wananipenda na wanasali kwa ajili yangu.

Paulo mara kwa mara alianza nyaraka zake kwa kuonyesha upendo kwa waumini wa Kanisa na kuwaambia kwamba alisali kwa ajili yao. Fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia watoto kuelewa kwamba viongozi wao wa Kanisa wanawapenda.

Shughuli Yamkini

  • Soma Wafilipi 1:3–4 na Wakolosai 1:3 9 kwa sauti, na waombe watoto kukunja mikono yao na kuinamisha vichwa vyao kila wakati wanaposikia maneno sali, kusali, na sala. Eleza kwamba Mtume Paulo alisali kwa ajili ya waumini wa Kanisa, kama vile viongozi wetu wa Kanisa wanavyosali kwa ajili yetu leo.

  • Onyesha picha ya Yesu Kristo, na shiriki mifano ya Yeye akisali kwa ajili ya mtu fulani (ona Luka 22:32; 3 Nefi 19:21, 23). Yesu aliomba nini wakati alipoomba kwa ajili ya wengine?

  • Wasaidie watoto kutaja majina ya baadhi ya viongozi wao wa Kanisa, kama vile rais wa Msingi, askofu, na Rais wa Kanisa. Eleza kwamba viongozi hawa wanamwomba Baba wa Mbinguni kuwabariki watoto na kuwasaidia kuishi kwa haki. Fikiria kuwaeleza watoto kile unasema wakati unaposali kwa ajili yao.

Wafilipi 4:4, 8

Ninaweza kufurahi katika Bwana.

Paulo aliwatia moyo Watakatifu kufurahi—hata kama walikabiliwa na majaribu magumu na Paulo mwenyewe alikuwa kifungoni. Utawasaidia vipi watoto waone kwamba kuishi injili kunaleta furaha?

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto wasikilize neno lililorudiwa wakati unaposoma Wafilipi 4:4. Waombe watoto wakuoneshe kile ambacho wanaweza kufanya wanapofurahi. Wasaidie kuelewa kwamba “kufurahi katika Bwana” inamaanisha kuhisi furaha kwa sababu tuna injili na kwa sababu Yesu Kristo anatupenda.

  • Lete vitu au picha ambazo zinawakilisha vitu ambavyo vinakusaidia “kufurahi katika Bwana.” Unaweza kuleta uumbaji wa kupendeza wa Mungu au picha ya hekalu, Mwokozi aliyefufuka, au familia. Waache watoto wachukue zamu kuchagua picha au kitu, na kisha waelezee kwa nini kinakufanya uwe na furaha. Waalike kuelezea vitu ambavyo vinawasaidia wao kufurahia katika Bwana.

  • Someni Wafilipi 4:8 pamoja, na wasaidie watoto kufikiria juu ya vitu ambavyo vinaendana na maelezo katika aya (ona pia Makala ya Imani 1:13). Wape watoto vipande vya karatasi na waache wachore picha za vitu hivi kuwasaidia “kufikiria juu ya” vitu ambavyo Paulo alielezea.

Wakolosai 1:23; 2:6–7

Imani yangu inapaswa “kukita mizizi” katika Yesu Kristo.

Kama watoto wanaweza kujenga maisha yao na imani yao juu ya Mwokozi, watakuwa na uwezo wa kustahimili dhoruba za maisha.

Shughuli Yamkini

  • Onyesha picha ya mti kutoka muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia unaposoma virai muhimu kutoka Wakolosai 1:23; 2:6–7. (Au Onyesha video ”Spiritual Whirlwinds” kwenye LDS.org.) Je, nini kingetokea kwa mti huu kama dhoruba ingekuja na mti haukuwa na mizizi imara? Waache watoto wasimame na wajifanye kuwa mti ambao una mizizi dhaifu katika dhoruba na kisha mti wenye mizizi imara. Ni kwa jinsi gani imani katika Mwokozi inaweza kutusaidia kuwa kama mti wenye mizizi imara?

  • Mualike mtoto kuchora mti ubaoni. Waombe watoto kutaja baadhi ya vitu wanavyoweza kufanya kuwa na “mizizi” katika Yesu Kristo. Kila wakati mtoto anapotaja kitu fulani, mtake yeye kuongeza mzizi kwenye mchoro.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

Wafilipi 4:4–13

Kama nina imani katika Yesu Kristo, ninaweza kuwa na furaha hata wakati wa shida.

Paulo aliteseka na majaribu mengi, lakini alikuwa na furaha kwa sababu alikuwa na imani katika Yesu Kristo.

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto wafikirie kwamba wako gerezani, kama vile Mtume Paulo alivyokuwa wakati alipoandika waraka kwa Wafilipi. Soma Wafilipi 4:4–13 pamoja na watoto na waombe watafute maneno yafuatayo: kufurahi, amani, ridhika. Je, ni kwa nini Paulo aliweza kufurahi na kuhisi amani hata akiwa gerezani? Wasaidie watoto kutafuta maneno Bwana, Mungu, na Kristo katika mistari hii. Wasaidie kuelewa kwamba imani ya Paulo katika Yesu Kristo ilifanya iwezekane kwake yeye kufurahi.

  • Waalike watoto wakusaidie kukamilisha sentensi kama zifuatavyo: ninaweza kuwa katika giza na bado nikaona kama nina . Ninaweza kuwa nje siku ya joto kali na bado nikahisi ubaridi kama nina Ninaweza kuwa na shida na bado nikapata furaha kama nina . Wasaidie watoto kufikiria njia wanazoweza kupata furaha katika Yesu Kristo wakati wanapokuwa na wakati mgumu. Wanaweza kuimba wimbo, kusoma maandiko wanayoyapenda, kumhudumia mtu fulani, au kusali sala ya shukrani. Je, Wafilipi 4:4–13 inapendekeza nini? Shiriki na watoto baadhi ya nyimbo au maandiko ambayo yanakusaidia wewe kupata furaha katika nyakati za shida.

Wafilipi 4:8

Ninaweza kufikiria juu ya vitu ambavyo ni vya kweli, aminifu, na safi.

Watoto mara kwa mara wanahatarishwa kwenye vitu ambavyo ni viovu na vichafu. Unaweza kuwasaidia kutafuta vitu vyenye kutia moyo na visafi.

Shughuli Yamkini

  • Mwombe mtoto mmoja asome Wafilipi 4:8 kwa sauti wakati wengine wanatafuta maneno katika Makala ya Imani 1:13 ambayo ni sawa au yanafanana. Mwalike mtu fulani kuandika maneno haya ubaoni. Toa ufafanuzi rahisi wa maneno haya na waombe watoto wafananishe ufafanuzi na maneno. Je, ni kwa nini tunapaswa “kutafakari juu” ya mambo haya? Tunawezaje “kuyatafuta” hayo?

  • Waombe watoto kutaja vitu ambavyo vinaweza kuwa sawa na maelezo katika Wafipilipi 4:8. Waalike kuweka orodha wiki hii ya kila kitu wanachokiona ambacho kinaendana maelezo haya. Wahimize kuleta orodha zao kwenye darasa la Msingi wiki ijayo na kuelezea kile walichopata.

Wakolosai 1:23; 2:6–7

Imani yangu inapaswa “kukita mizizi” katika Yesu Kristo.

Shetani anajaribu kudhoofisha imani ya watoto kupitia majaribu na mafundisho ya uongo. Je, ni kwa namna gani unaweza kuwapa watoto mwongozo wa kiungu ili kuimarisha imani yao katika Mwokozi ili kwamba “wasigeuzwe kuliacha tumaini la injili”?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kuchora picha ambazo zinawakilisha ukweli wanaoupata katika Wakolosai 1:23; 2:6–7. Waache washiriki picha zao pamoja na darasa na kueleza ukweli unaowakilishwa na picha zao.

  • Onyesha video ”Spiritual Whirlwinds.” Je, baadhi ya majaribu na maandiko ya uongo ulimwenguni leo ambayo huweza kudhoofisha imani yetu ni yapi? Je, tunaweza kufanya nini ili kuimarisha imani yetu ili kwamba tuwe “tumekita mizizi” katika Yesu Kristo?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki pamoja na familia zao kile walichojifunza kuhusu “kukita mizizi” katika Kristo. Wanaweza kutumia ukurasa wa shughuli wa wiki hii au maandiko waliyosoma darasani leo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Watoto ni wadadisi na wanajifunza kupitia uzoefu mpya na tofauti. Tumia shughuli zinazowasaidia watoto kusogea sogea, kutumia milango yao yote ya hisi, kuchunguza, na kujaribu vitu vipya. Mapendekezo katika “Kukidhi Mahitaji ya Watoto Wadogo” mwanzoni mwa nyenzo hii yanaweza kusaidia. (Ona pia Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.)

Chapisha