Njoo, Unifuate
Oktoba 14–20. Wafilipi; Wakolosai: ‘Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu’


“Oktoba 14–20. Wafilipi; Wakolosai: ‘Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye Nguvu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019 (2019)

“Oktoba 14–20. Wafilipi; Wakolosai,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Paulo akiandika barua kutokea gerezani

Oktoba 14–20

Wafilipi; Wakolosai

“Nayaweza Mambo Yote katika Kristo Anitiaye nguvu”

Ni lini ilikuwa mara ya mwisho wewe kusoma misukumo ya kiroho uliyoandika wakati wa kujifunza kwako Agano Jipya? Inaweza kusaidia kupitia tena ushawishi ambao umekuwa ukiupata.

Andika Misukumo Yako

Paulo aliandika nyaraka zake kwa Wafilipi na Wakolosai wakati akiwa gerezani. Lakini barua hizi hazina toni unayoweza kutegemea kutoka kwa mtu aliye gerezani. Paulo aliongea zaidi kuhusu furaha, kushangilia, na kutoa shukrani kuliko alivyofanya kuhusu mateso na majaribu: “Kristo anahubiriwa,” alisema, “na kwa hiyo nafurahi, naam, nami nitafurahi” (Wafilipi 1:18). “Maana Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho, nikifurahi na kuuona … uthabiti wa imani yenu katika Kristo” (Wakolosai 2:5). Kwa hakika, “amani ya Mungu” ambayo Paulo aliipata katika hali zake ngumu “hupita akili zote” (Wafilipi 4:7), lakini ilikuwa hata hivyo ni uhalisia. Katika majaribu yetu wenyewe, tunaweza kujisikia wenye amani sawa na hii na “kufurahi katika Bwana siku zote” (Wafilipi 4:4). Tunaweza, kama Paulo alivyofanya, kutegemea kikamilifu kwa Yesu Kristo, “ambaye katika yeye tuna ukombozi” (Wakolosai 1:14). Tunaweza kusema, kama Paulo alivyosema “Nayaweza mambo yote katika Kristo anitiaye nguvu” (Wafilipi 4:13; ona pia Wakolosai 1:11).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Wafilipi 2:12–13

Je “tunatimiza wokovu [wetu] wenyewe”?

Kirai “utimizeni wokovu wenu wenyewe” kinatumiwa na baadhi ya watu kuunga mkono wazo kwamba tunaokolewa tu kwa juhudi zetu wenyewe. Lakini huo ni mtazamo finyu, kama ilivyo finyu kuelewa fundisho la Paulo—mnaokolewa kwa neema kwa njia ya imani” (Waefeso 2:8)—kumaanisha kwamba hakuna matendo yanayohitajika ili kupata wokovu. Maandiko, ikijumuisha maandishi ya Paulo, kwa uwazi yanafundisha umuhimu wa vyote viwili neema ya Yesu Kristo na juhudi binafsi ili kupokea wokovu. Kama Nefi alivyosema, “Ni kwa neema kwamba tunaokolewa, baada ya kutenda yote tunayoweza” (2 Nefi. 25:23). Hata katika juhudi zetu za kutimiza wokovu wetu wenyewe, “ni Mungu atendaye kazi ndani yenu” (Wafilipi 2:13; ona pia Wafilipi 1:6; Kamusi ya Biblia, “Neema”).

Wafilipi 3:5–14

Injili ya Yesu Kristo inastahili kila dhabihu.

Paulo aliacha vingi wakati alipoongoka kwenye injili ya Yesu Kristo, ikiwemo nafasi mashuhuri aliyokuwa nayo katika jumuiya ya Wayahudi kama Mfarisayo. Katika Wafilipi 3:5–14, tafuta Paulo alipata nini kwa sababu alikuwa radhi kujitoa dhabihu kwa ajili ya injili. Je, ni kwa jinsi gani alijisikia kuhusu dhabihu yake?

Kisha fikiria ufuasi wako mwenyewe. Je, wewe umetoa dhabihu gani kwa ajili ya injili ya Yesu Kristo? Je, wewe umepokea nini? Je, kuna dhabihu yoyote ya ziada unayohisi unahitajika kufanya ili kuwa mfuasi wa Mwokozi aliyejitoa kikamilifu?

Ona pia 3 Nefi 9:19–20; Mafundisho na Maagano 58:2–5; Robert C. Gay, “Mwanadamu Atatoa Nini Badala ya Nafsi Yake?” Ensign au Liahona, Nov. 2012, 34–36.

Wafilipi 4:1–13

Ninaweza kupata furaha kwa Kristo, bila kujali hali yangu.

Maisha ya Paulo ni kielelezo halisi cha ukweli ulioelezewa na Rais Russell M. Nelson: “Wakati fokasi ya maisha yetu inapokuwa katika … Yesu Kristo na injili Yake, tunaweza kujisikia wenye furaha bila kujali nini kinatokea—au kisichotokea—katika maisha yetu. Furaha huja kutoka kwa na kwa sababu Yake” (“Furaha na Kuendelea Kusalia Kiroho,” Ensign au Liahona, Nov. 2016, 82).

Unaposoma Wafilipi—hasa sura ya 4—tafuta kauli zinazoweza kukusaidia kupata furaha katika hali yo yote ya maisha yako. Je, ni lini umepata kuonja “amani ya Mungu” wakati wa changamoto? (mstari wa 7). Ni lini umepata nguvu “katika Kristo” kufanya mambo magumu? (mstari wa 13). Kwa nini unafikiri ni muhimu “kuwa mwenye kuridhika” katika hali zote? (mstari wa 11). Je, ni kwa jinsi gani kufanyia mazoezi sifa katika mstari wa 8 hukusaidia kupata furaha katika hali zako?

Ona Alma 33:23; Dieter F. Uchtdorf, “Shukuru katika Hali Zozote,” Ensign au Liahona, Mei 2014, 70–77.

Wakolosai 1:12–23

Imani yangu iko juu ya Yesu Kristo.

Hapa kuna mbinu ya kujifunza unayoweza kujaribu kwenye karibia kila sura ya maandiko, ingawa inafanya kazi vizuri zaidi kwenye Wakolosai 1:12–23. Tafuta mistari kwa ajili ya chochote unachojifunza kuhusu Yesu Kristo, na tengeneza orodha ya kile unachopata. Kwa nini unahisi ni muhimu kujua mambo haya kuhusu Mwokozi?

Wakolosai 3:1–17

Wafuasi wa Yesu Kristo hufanywa “upya” pale wanapoishi injili Yake.

Je, ni kwa jinsi gani unajua kama injili ya Yesu Kristo inakusaidia kuwa “mtu mpya”? Njia mojawapo ya kujua ni kutafiti Wakolosai 3:1–17 na kutengeneza orodha ya mitazamo, sifa, na matendo ya “mtu wa kale” na orodha nyingine ya mitazamo, sifa, na matendo ya “mtu mpya.”

Je, kujifunza kwako mistari hii kunakupa mwongozo wa kiungu wa mawazo yoyote kuhusu jinsi gani injili inavyokubadilisha? Andika mawazo yako ili kwamba uweze kuyapitia tena baadaye na tafakari jinsi gani unavyokua.

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Hapa kuna baadhi ya mapendekezo:

Wafilipi

Familia yako inaweza kugundua maneno furaha au shangilia yakirudiwa mara kwa mara katika Wafilipi. Kila mara mnapokutana na moja ya maneno haya, mnaweza kusimama na kujadili Paulo alifundisha nini kuhusu jinsi ya kuwa na furaha.

Wafilipi 2:14–15

Ni kwa jinsi gani tunaweza “kuangaza kama nuru katika ulimwengu”?

Wafilipi 4:8.

Pengine familia yako wanaweza kuonyesha mambo ya “kutafakari” ambayo yanaendana na maelezo katika mstari huu (ona pia Makala ya Imani 1:13). Ni kwa jinsi gani familia yako itabarikiwa kwa kufuata ushauri wa Paulo?

Wakolosai 1:9–11; 2:2–3

Je, tunaweza kufanya nini ili tuzidi “katika maarifa ya Mungu”? Je, “hazina za hekima na maarifa” tunazopata katika injili ni zipi?

Wakolosai 1:23; 2:7

Pengine familia yako inaweza kusoma mistari hii wakiwa wamekaa kuzunguka mti au wakiwa wanaangalia picha ya mti (kama ile ya mti ambayo inaambatana na muhtasari huu). Inamaanisha nini “kujengwa” na “kuwa na shina” katika Kristo? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kusaidiana sisi kwa sisi kuimarisha mashina yetu ya kiroho?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Ishi ushuhuda wako. “Unafundisha kile ulicho,” Mzee Neal A. Maxwell alifundisha. “Sifa zako zitakumbukwa zaidi … kuliko kweli fulani katika somo fulani” (katika Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 13).

Picha
mti

Paulo alifundisha kwamba imani yetu inapaswa “kuwa na shina” katika Yesu Kristo (Wakolosai 2:7).

Chapisha