2011
Matokeo mema katika Kuumwa na Mbwa
Machi 2011


Vijana

Matokeo mema katika Kuumwa na Mbwa

Katika majira ya joto ya 2009, niliumwa usoni na mbwa wa rafiki yangu. Bahati mbaya midomo yangu ilipasuliwa, na ilinibidi nishonwe.

Kwa sababu ya kuumizwa huku, nilivunjika moyo sana. Nilikubali dhiki ichukue mawazo yangu, na nikahisi kama maisha yangu yote kama yameharibiwa. Nilikuwa nikiwaza sana juu ya midomo yangu na sikutaka kuenda nje kwenye umma hata kidogo. Katika akili yangu mipango yangu ya kupiga kinanda, voliboli, kanisa, kuogelea, na shule ilivunjwa na kuumizwa kwangu.

Lakini wakati wowote nilipoomba, na kupokea baraka za ukuhani, nilipoongea na wazazi wangu, au nilipotembelewa na wanafamilia na marafiki, roho yangu iliinuliwa na kuhisi furaha katika wakati wa huzuni. Punde nilitambua kwamba kama watu walijali kuumizwa kwangu, walikuwa wanahisi huruma.

Huu uzoefu ulinisaidia kujenga hulka yangu, na nikajifunza kutojali kuhusu kile watu wengine walivyofikiria juu yangu. Pia nilibarikiwa kwa sababu kuumizwa kwangu kulinisaidia kutambua kwamba ninafaa kujifikiria kidogo sana na kuanza kuwashughulikia wengine. Roho yangu iliimarishwa sana wakati huu.

Nilijifunza kwamba dhiki ni sehemu ya mpango wa Baba wa Mbinguni kwetu. Kama tutatafuta wema na sio ubaya, tunaweza kushinda dhiki, kuwa watu bora, na kuacha uzoefu huo kuimarisha ushuhuda wako.

Chapisha