2014
Nilihudumu tena
Septemba 2014


Vijana

Nilihudumu tena

Mwandishi anaishi Rio Grande do Norte, Brazil.

Siku moja, baada ya kukamilisha mradi wa huduma, nilikuwa nikitembea mbele ya jumba la mikutano na nikawaona dada wawili waliokuwa wakisafisha jengo. Meneno yangu yalitoka tu: “Akina dada, mnahitaji msaada?” Mmoja wao alitabasamu kwangu na kusema kwamba nilikuwa nimefika kwa wakati mzuri kwa sababu walikuwa ni wao pekee waliokuwa wanasafisha na walikuwa wamechoka. Alisema kwamba alikuwa ameomba kuwa Bwana angetuma mtu kuwasaidia. Nilifurahi sana mimi kuwa jibu la maombi yake. Nilikuwa nimemaliza tu kutoa huduma kwa mtu mwingine na nilikuwa nimechoka, lakini nilifuata moyo wangu na kujitolea kuhudumu zaidi.

Ni amri kufanya kazi kwa shangwe (ona M&M 24:7). Tunapokuwa na hamu ya kuhudumu nyakati zote, tunaweza kusaidia kufanya miujiza itendeke katika maisha ya watu wengine. Maisha yetu yanakuwa na maana zaidi tunapohudumu. Bwana kwa kweli anatupenda, Yeye husaidia kila mmoja wa watoto wake na atatupa nguvu za kuhudumu.

Chapisha