Agano Jipya 2023
Juni 11. Ni kwa Jinsi Gani Ninaweza Kuzidi Kuwa Karibu na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo? Yohana 14–17


“Juni 11. Ni kwa Jinsi Gani Ninaweza Kuzidi Kuwa Karibu na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo? Yohana 14–17,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Akidi za Ukuhani wa Haruni na Madarasa ya Wasichana: Mada za Mafundisho 2023 (2022)

“Juni 11. Ni kwa Jinsi Gani Ninaweza Kuzidi Kuwa Karibu na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Akidi za Ukuhani wa Haruni na Madarasa ya Wasichana: Mada za Mafundisho 2023

Picha
msichana akisali

Juni 11

Ni kwa Jinsi Gani Ninaweza Kuzidi Kuwa Karibu na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?

Yohana 14–17

Picha
ikoni ya kushauriana kwa pamoja

Shaurianeni kwa Pamoja

Ikiongozwa na mshiriki urais wa darasa au akidi; takribani kwa dakika 10–20

Mwanzoni mwa mkutano, rudieni kwa pamoja Dhima ya Wasichana au Dhima ya Akidi ya Ukuhani wa Haruni. Kisha ongoza mjadala kuhusu kazi ya wokovu na kuinuliwa ukitumia swali moja ua mengi ya yale yaliyopo hapo chini au yako mwenyewe (ona Kitabu cha Maelezo ya Jumla, 10.2, 11.2). Panga njia za kutenda juu ya kile mnachojadili.

  • Ishi injili. Je, ni uzoefu gani ya hivi karibuni umeimarisha shuhuda zetu?

  • Kuwajali wenye mahitaji. Je, ni akina nani wanahitaji msaada wetu na sala zetu? Je, ni nini tunahisi kuvutiwa kukifanya ili kusaidia?

  • Waalike wote kuipokea injili. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwa nuru kwa wanafamilia au marafiki ambao hawashiriki imani yetu?

  • Unganisha familia milele. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuonyesha upendo zaidi na ufadhili kwa familia zetu na kuleta tofauti chanya katika nyumba zetu?

Mwishoni mwa somo, kama inafaa, fanya yafuatayo:

  • Shuhudia juu ya kanuni zilizofundishwa.

  • Wakumbushe washiriki wa darasa au akidi kuhusu mipango na mialiko iliyotolewa wakati wa mkutano.

Picha
ikoni ya kufundisha mafundisho

Fundisha Mafundisho

Mkiongozwa na kiongozi mtu mzima au kijana; takribani kwa dakika 25–35

Jiandae Binafsi Kiroho

Tunda haliwezi kukua kwenye tawi ambalo limetengana na mti wake. Kwa njia hiyo hiyo, hatuwezi kukua kiroho kama tumetenganishwa na Mungu (ona Yohana 15:4–6). Kuna nguvu nyingi sana ambazo zinajaribu kututenganisha Naye—wakati mwingine kiburi chetu wenyewe au chaguzi mbaya lakini mara nyingi ni hali za maisha ya duniani. Wakati Yesu alipokutana na wafuasi Wake kwa mara ya mwisho hapa duniani, Yeye alijua kwamba punde angetenganishwa nao. Kwa hiyo aliwafundisha kuhusu umuhimu wa kuwa na muunganiko wa karibu Naye na Baba Yake—kwa kuwa wameunganika nao kama vile tawi lilivyo na mti. Aliita hili “kubaki” ndani Yake. Na aliwafundisha wanafunzi Wake jinsi ya kufanya hivyo. Muhimu zaidi ya yote, kupitia dhabihu Yake ya upatanisho, Yeye alifanya muunganiko huo kuwezekana.

Tafakari muunganiko wako na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wakati unapojifunza Yohana 14:17. Fikiria pia kuhusu watu unaowafundisha na matamanio yao ya kuwa karibu na Mungu. Je, utafanya nini ili kuwasaidia? Ungeweza kutafakari Mafundisho na Maagano 88:62–68 unapojiandaa kufundisha.

Jifunzeni Pamoja

Fikiria jinsi ungeweza kuwashawishi vijana kujadili mafundisho ya Mwokozi juu kuhusu mzeituni na matawi katika Yohana 15:1–12. Pengine ungeweza kutumia mchoro, picha, au tawi halisi ili kuwasaidia kupiga taswira kile Yesu alifundisha. Ungeweza kuwaomba wazungumze kuhusu nyakati walipohisi kuwa karibu na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo—au nyakati walipohisi kuwa mbali na wao. Mistari hii inafundisha nini kuhusu jinsi tunavyoweza kukaa karibu Nao? Shughuli kama hii ifuatayo inaweza kusaidia kudumisha mazungumzo.

  • Ingekuwa ya thamani kutumia muda fulani kuchunguza swali “Ni nini kinatuweka mbali na Baba wa Mbingu na Yesu Kristo?” Ungeweza kuandika swali hili ubaoni na kuomba majibu. Labda ungeweza kisha kuzungumza kuhusu kile tunachofanya ili kujenga uhusiano na rafiki au mwanafamilia. Ni kwa jinsi gani hii inafanana—na ni tofauti na—njia tunayojenga mahusiano na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo? Ni kwa jinsi gani Yesu Kristo anatusaidia sisi kusogea Kwake na Baba Yake? Wahimize washiriki wa darasa au akidi kusoma maandiko katika “Nyenzo Saidizi” ili kuwasaidia wao kujibu sali hili. Vijana wangeweza kunufaika kutokana na kujifunza mistari hii na kushiriki kile wamejifunza.

  • Hakuna aliye karibu na Mungu Baba kuliko Mwana Wake Mpendwa, Yesu Kristo. Tunaweza kujifunza nini kutokana na Mwokozi kuhusu kusogea karibu na Mungu? Washiriki wa darasa na akidi wangeweza kutafakari swali hili wanaposoma Luka 22:41–43; Yohana 6:38; 17:3, 20–23; 3 Nefi 11:11; Mafundisho na Maagano 50:43. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwa wamoja na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?

  • Katika ujumbe wake “Mwokozi Wetu Binafsi,” Mzee Michael John U. Teh anakumbuka wakati alitambua, “Kile ninachojua kuhusu Mwokozi kimeshindwa sana jinsi kweli ninavyomjua Yeye” (Liahona, Mei 2021, 99). Ungeweza kuomba darasa lako au akidi yako kujadili tofauti kati ya kujua kuhusu Yesu Kristo na kumjua Yeye kihalisi. Wangeweza kuzungumza kuhusu kile wanachofanya ili kujua kuhusu Yeye na kile wanachofanya ili kumjua Yeye kweli. Wangeweza kisha kupekua sehemu za ujumbe wa Mzee Teh ili kupata ushauri alioutoa kuhusu kuja kumjua Mwokozi. Je, ni kwa jinsi gani sisi tumebarikiwa kwa kutafuta kumjua Yeye?

  • Katika video “He Knows Me,” vijana wawili kutoka Ghana wanaelezea juhudi za kusogea karibu na Mungu. Pengine washiriki wa darasa au akidi wangeweza kutazama video hiyo na, kutengeneza orodha ya mawazo inayowapa kuhusu jinsi ya kuboresha mahusiano yao na Baba yao wa Mbinguni. Waalike kushiriki kitu fulani kutoka katika orodha zao. Kama inawezekana, wangeweza kufurahia kutengeneza video zao fupi zikielezea jinsi wao wanasogea karibu na Mungu.

Picha
wasichana wakisoma maandiko

Tunapokuja kumjua Mwokozi na kutii amri Zake, tutakaa ndani ya upendo Wake (ona Yohana 15:10).

Tenda kwa Imani

Watie moyo washiriki wa darasa au akidi kutafakari na kuandika kile watakachofanya juu misukumo waliyoipokea leo. Kama wangependa, wangeweza kushiriki mawazo yao. Waalike wafikirie kuhusu jinsi kutenda juu ya misukumo yao kutaimarisha mahusiano yao na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Nyenzo Saidizi

Kufundisha katika Njia ya Mwokozi

Mwokozi alijiandaa kwa huduma Yake ya duniani kwa kusali na kufunga ili kwamba angeweza kuwa karibu na Baba Yake (ona Mathayo 4:1–2; Luka 4:1–2). Unapojiandaa kufundisha, chukua muda kutafuta mwongozo wa Baba wa Mbinguni, kwani unawafundisha watoto Wake!

Chapisha