Njoo, Unifuate
Mikutano ya Jumapili ya Nne


Mikutano ya Jumapili ya Nne

Jumapili ya nne ya kila mwezi, akidi ya wazee, na Muungano wa Usaidizi wa Wakina Mama watajadili mada iliyochaguliwa na Urais wa Kwanza na Akidi ya Mitume Kumi na Wawili. Mada ya Jumapili ya nne itatengenezwa upya baada ya kila mkutano mkuu. Kutoka sasa hadi mkutano mkuu ujao, mada itakuwa “Kuwatumikia wengine.” Kila mwezi,viongozi au walimu wanaweza kuchagua kuongoza majadiliano juu ya kanuni yo yote kati ya zifuatazo zenye uhusiano na utumishi.

Je, kutumikia kuna maana gani?

Je, utumishi inamaanisha nini kwa waumini katika kata yako au tawi? Ili kupata jibu, unaweza kuandika Utumishi ubaoni na kisha waalike washiriki waandike maneno kulizunguka ambayo wanayahusisha na utumishi. Washiriki wanaweza kupata maneno au virai ili kuongezea kwenye orodha kutoka kwenye maandiko kama yafuatayo: Mathayo 25:34–40; Luka 10:25–37; 2 Nefi 25–26; Mosia 18:8–9; 3 Nefi 18:25; na Mafundisho na Maagano 81:5. Tunajifunza nini kutoka kwenye mistari hii kuhusu utumishi? Unaweza kuwaomba washiriki kushiriki mifano ya utumishi waliyoiona. Je, ni kwa jinsi gani utumishi wetu unaweza kukidhi mahitaji ya watu kiroho na kimwili? Inawezaje kuwasaidia watu kumkaribia zaidi Kristo?

Mwokozi ndiye mfano wetu kamili wa utumishi.

Ili kujifunza kuhusu jinsi ya kutumikia vyema, washiriki wanaweza kushiriki hadithi kutoka maandiko ambapo Mwokozi aliwatumikia wengine—mifano kadhaa inaweza kupatikana katika Yohana 4–6 na Marko 2:1–12. Washiriki wanaweza kushiriki kile kinachowavutia kuhusu hadithi hizi na kanuni gani wanazojifundisha kuhusu utumishi. Kwa mfano, ni kwa jinsi gani Mwokozi alibinafsisha huduma Yake kwa wengine? Je, ni kwa jinsi gani aliweza kukidhi mahitaji ya watu ya kiroho na vile vile ya kimwili? Washiriki wa darasa wanaweza kuelezea wakati ambapo waliwaona watu wakitumia kanuni hizi katika utumishi wao.

Utumishi unahamasishwa na upendo kama wa Kristo.

Kuchunguza nguvu ya utumishi uliohamasishwa na upendo kama wa Kristo, unaweza kuandika sentensi zifuatazo ubaoni na waombe washiriki kupendekeza njia za kujaza mapengo: Hakika ninapowapenda watu ninaowahudumia, mimi . Ninapohudumia kwa sababu zingine, mimi . Je, tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kuwa utumishi wetu kwa wengine unahamasishwa na upendo kama wa Kristo? Tunawezaje kujenga upendo kama wa Kristo kwa wale ambao tumepangiwa kuwatumikia? [ona Moroni 7:45–48). Pengine waumini wanaweza kutoa mifano ya utumishi ambao ulitiwa msukumo na upendo kama wa Kristo.

Mungu anataka watoto Wake wote kulindwa na kutunzwa.

Rais Russell M. Nelson alisema, “Sifa bainifu ya Kanisa la kweli na lililo hai la Bwana daima itakuwa ni jitihada zenye utaratibu, zilizoelekezwa kuwatumikia watoto wa Mungu mmoja mmoja na familia zao” (“Kutumikia kwa Nguvu na Mamlaka ya Mungu,” Liahona, Mei 2018, 69) Rais Nelson anafundisha zipi ni baadhi ya njia “zilizopangwa, kuelekezwa” ambazo kwazo Kanisa linatusaidia sisi kutoa utunzaji mzuri zaidi kwa watu binafsi? Kwa nini juhudi hizi “ni sifa bainifu za Kanisa la kweli na lililo hai”? (ona Mosia 18:21.-22 na Moroni 6:4-6 kwa ajili ya baadhi ya mawazo). Ni baraka gani zimekuja katika maisha yetu au maisha ya wengine kwa sababu watu walitumikia katika miito au kazi yao ya Kanisa?

“Thamani ya nafsi ni kubwa machoni mwa Mungu.

Uzoefu wa wana wa Mosia unaonesha kwamba njia tunayowaona watu inaathiri jinsi tunavyowatumikia. Unaweza kuandika ubaoni Jinsi Wanefi walivyowaona Walamani na Jinsi wana wa Mosia walivyowaona Walamani. Kisha waalike washiriki wapekue Mosia 28:1–3 na Alma 26:23–26 ili kutafuta maneno na virai vya kuandika chini ya kauli hizi. Mfananisho huu unatufundisha nini kuhusu jinsi gani tunayowaona watu inavyoathiri njia tunayowatumikia? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kujifunza kuwaona watu zaidi kama Mungu anavyowaona? (ona M&M 18:10–16.

Watumishi wa kweli wanalenga kwenye mahitaji ya wengine.

Kuwasaidia washiriki waelewe vyema thamani ya kulenga kwenye mahitaji ya wengine tunapowatumikia, unaweza kufananisha utumishi na kutoa na kupokea zawadi. Je, tumewahi kupokea zawadi ya maana kutoka mtu fulani ambaye kwa uwazi alijua nini tulihitaji au kutaka. Je, ni jinsi gani utumishi ni sawa na kutoa zawadi ya sahihi? Fikiria kujadili hadithi kutoka kwenye mkutano mkuu wa hivi karibuni ambazo zilionesha jinsi watu walivyotumikia kulingana na mahitaji ya wengine (ona, kwa mfano, Jean B. Bingham, “Kutumikia kama Mwokozi Afanyavyo,” Liahona, May 2018). Washiriki wanaweza pia kushiriki hadithi zingine ambazo zinaonesha kanuni hii.

Ni kwa jinsi gani tunaweza kujifunza ni nini mahitaji ya wengine? Mwalike kila mshiriki kutengeneza orodha ya baadhi ya watu ambao wanawatumikia. Kando ya kila jina wanaweza kuandika jibu kwa swali “mtu huyu anahitaji nini kumkaribia zaidi Kristo?” Kama inavyotakiwa, watie moyo washiriki kujumuisha ibada kila mtu anayoweza kuhitaji kupokea. Waalike washiriki kuendelea kufikiri kuhusu swali hili na watafute mwongozo wa kiungu ili kuwasaidia kukidhi mahitaji ya wengine.

Bwana anatutaka tukubali utumishi kutoka kwa wengine.

Mzee Robert D. Hales alisema: “Mpango wa injili unahitaji kutoa na kupokea. … Watu wenye matatizo mara nyingi wanasema: ‘Nitafanya mwenyewe,’ … ‘Ninaweza kujitunza mwenyewe.’ Imesemwa kwamba hakuna ambae ni tajiri mno kiasi kwamba hahitaji msaada wa mwingine, hakuna masikini sana kiasi kwamba hawezi kuhitajika katika njia fulani kwa mwanadamu mwenziwe. Tabia ya kuomba msaada kutoka kwa wengine kwa kujiamini, na kukubali kwa huruma, inapaswa kuwa ni sehemu ya asili yetu” (“We can’t Do it Alone,” Ensigh, Nov. 1975 91,93). Kwa nini wakati mwingine tunasita kukubali msaada kutoka kwa wengine? Ni kwa jinsi gani utayari wetu kukubali msaada huwabariki wale wanaotuhudumia? Wape washiriki muda mfupi kutafakari juu ya njia ambazo wanazoweza kuwa wawazi zaidi ili kupokea utumishi wa wengine. Je, 1 Wakorintho 12:13–21 inapendekeza nini kuhusu kwa nini tunategemeana?

Kuna njia nyingi tunazoweza kuwatumikia wengine.

Kuwasaidia washiriki kufikiria njia nyingi tunazoweza kutumikiana sisi kwa sisi, unaweza kuwaalika kurejea upya ujumbe wa Mzee Jeffrey R. Holland “Kuwa Pamoja na Kuwaimarisha” (Liahona, Mei 2018, 101–3; ona pia “Kanuni za Utumishi” katika matoleo yajayo ya Liahona). Washiriki wanaweza kugawanyika katika makundi madogo madogo, na kila kikundi kinaweza kufikiria hali kadhaa ambazo mtu anaweza kuhitaji msaada. Kisha wanaweza kutafuta mbinu za kutatua matatizo katika njia mbalimbali ambazo watu wanaweza kutumikia kwa mahitaji ya kiroho na kimwili ya watu binafsi katika hali hizo tofauti. Yaombe makundi kutoa mawazo yao na kutafakari kama wazo lolote lililojadiliwa linaweza kubariki watu ambao wanawatumikia.

Chapisha