Njoo, Unifuate
Desemba 7–13. Moroni 7–9: “Kristo Akuinue Juu”


“Desemba 7–13. Moroni 7–9: ‘Kristo Akuinue Juu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Desemba 7–13. Moroni 7–9,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2020

Picha
Moroni akiandika kwenye bamba za dhahabu

Minerva Teichert (1888–1976), Moroni: Mnefi wa Mwisho, 1949–1951, mafuta kwenye masonite, inchi 34¾ x 47. Sanaa ya Jumba la Makumbusho la Chuo kikuu cha Brigham Young, 1969

Desemba 7–13

Moroni 7–9

“Kristo Akuinue Juu”

Kusoma kwa sala Moroni 7–9 kutaalika ushawishi wa Roho Mtakatifu. Atakusaidia kuelewa mahitaji ya watoto katika darasa lako.

Andika Misukumo Yako

Picha
Ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wakumbushe watoto kuhusu jambo ulilowaalika kufanya kipindi cha somo lililopita au jambo ambalo wanaweza kuwa wamejifunza na familia zao wiki hii. Waombe washiriki kile walichojifunza.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Moroni 7:33

Nikiwa na imani, ninaweza kufanya chochote Mungu anachohitaji nifanye.

Watoto walio na imani katika Yesu Kristo na ujasiri katika nguvu Zake wanaweza kufanya mambo makubwa pale wanapomtumikia Yeye.

Shughuli za Yakini

  • Soma Moroni 7:33, na waalike watoto kusimama kila mara wanaposikia neno “Imani.” Eleza kwamba tunaonyesha imani yetu katika Yesu Kristo kwa kutii amri Zake. Wasaidie watoto kutengeneza orodha ubaoni ya mambo Yesu anayowataka wafanye, kama kuwatii wazazi wao au kusema ukweli. Shuhudia kwamba imani yetu katika Yesu Kristo inaweza kutusaidia kutii amri.

  • Onyesha picha kadhaa ambazo zinaonyesha mtu katika Kitabu cha Mormoni (au vitabu vingine vya maandiko) akifanya jambo fulani muhimu kwa sababu alikuwa na imani katika Yesu Kristo (ona, kwa mfano, Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 19, 70, 7881). Wasaidie watoto kusimulia hadithi iliyoonyeshwa katika picha. Waambie kwamba kwa sababu watu hawa walikuwa na imani katika Yesu Kristo, walipewa nguvu ya kufanya kile Yeye alichowataka wafanye.

Moroni 7:41

Kuamini katika Yesu Kristo kunaweza kunipa tumaini.

Kuna watu wengi ulimwenguni ambao wanahisi kwamba hawana tumaini. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kupata tumaini katika Yesu Kristo?

Shughuli za Yakini

  • Soma na elezea Moroni 7:41 kwa watoto, na waombe kuinua mikono juu wakati wanaposikia jambo Mormoni alilosema tunapaswa kutumainia. Waambie watoto kuhusu tumaini unalohisi kwa sababu ya Yesu Kristo.

  • Waombe watoto kumfikiria mtu wanayemjua ambaye anapitia wakati mgumu kwenye jambo fulani. Waalike watoto kuchora picha kwa ajili ya mtu huyo ambayo inaweza kumkumbusha kuwa na tumaini katika Yesu Kristo.

Moroni 7:47

“Hisani ni upendo msafi wa Kristo.”

Ni uzoefu upi katika maisha yako ungeweza kuwasaidia watoto kujifunza kuwa wakarimu kwa wengine na kuwachukulia kwa upendo?

Shughuli za Yakini

  • Waombe watoto kurudia kifungu hiki cha maneno pamoja nawe: “hisani ni upendo msafi wa Kristo” (Moroni 7:47). Wasaidie watoto kufikiria njia ambazo Yesu Kristo alionyesha upendo kwa wengine (picha zingeweza kusaidia, kama vile Kitabu cha Sanaa ya Injili, kama vile na. 55, 83,84). Ni kwa jinsi gani Yeye ameonyesha upendo kwetu? Nani tunaweza kumwonyesha upendo kama Yesu alivyofanya? Kwa mfano, onyesha video “My Brother Hyrum” (ChurchofJesusChrist.org).

  • Waalike watoto kuchora picha zao wenyewe wakionyesha upendo kwa mtu mwingine. Pendekeza kwamba waweke picha zao mahali ambapo itawakumbusha wao kuwapenda wengine kama Yesu anavyowapenda wengine.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Moroni 7:21–22, 25, 33

Ninabarikiwa ninapokuwa na imani katika Yesu Kristo.

Mormoni alitaka watu wajue kwamba miujiza haikukoma wakati huduma ya Mwokozi duniani ilipofika mwisho. Kadiri tunavyokuwa na imani katika Yesu Kristo, tunaweza, kwa msaada Wake kufanya lolote Analohitaji tufanye—ikiwemo mambo ya kimiujiza.

Shughuli za Yakini

  • Wasaidie watoto kuorodhesha ubaoni baadhi ya “vitu vizuri” tunavyopokea kupitia injili ya Yesu Kristo, kama vile kuwa na familia za milele, kurudi kwa Baba wa Mbinguni, na kusamehewa dhambi zetu. Kisha waalike watoto wasome Moroni 7:21–22 na 25, wakitafuta jinsi tunavyoweza kupokea vitu hivi vyote vizuri. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuonyesha imani yetu katika Yesu Kristo na ahadi Zake?

  • Soma Moroni 7:33 kwa watoto, na waombe kusikiliza kile tunachoweza kufanya wakati tunapokuwa na imani katika Yesu Kristo. Kadiri inavyofaa, shiriki uzoefu uliowahi kuwa nao wakati imani ilipokusaidia kufanya kile Mungu alichotaka ufanye. Wasaidie watoto kufikiria na kushiriki mifano kutoka kwenye maisha yao. Ni kwa jinsi gani imani katika Kristo huleta tofauti katika mifano hii?

Moroni 7:40–41; 9:25–26

Ninaweza kuwa na tumaini katika Yesu Kristo, hata wakati wa majaribu magumu.

Mormoni na Moroni walikabiliwa na mazingira ya kukatisha tamaa, lakini walipata tumaini katika Mwokozi Yesu Kristo. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto kupata tumaini katika Kristo wakati wamekata tamaa?

Shughuli za Yakini

  • Wasaidie watoto kuorodhesha matatizo kadhaa ambayo yangeweza kuwafanya watu kuhisi kukata tamaa au kukosa tumaini. Waalike watoto wasome Moroni 7:40–41 na 9:25–26, wakitafuta jambo ambalo lingeweza kumsaidia mtu anayehisi kukata tamaa. Waambie jinsi Yesu Kristo na injili Yake vilivyokusaidia kipindi cha nyakati ngumu.

  • Waalike watoto waandike ujumbe kwa mtu anayehisi kukata tamaa ili kumsaidia kupata tumaini katika Kristo, kama Mormoni alivyofanya kwa mwanaye katika Moroni 9:25–26. Wahimize watoto kutumia maneno na vifungu vya maneno kutoka kwenye mistari hii katika jumbe zao.

  • Jaza chombo kitupu kwa maji, na dondosha vitu viwili ndani yake—kimoja kinachoelea na kingine kinachozama. Fananisha kitu kinachoelea na mtu mwenye tumaini katika Kristo. Someni pamoja Moroni 9:25. Ni kwa jinsi gani Kristo “hutuinua [sisi] juu” wakati tunapokabiliwa na majaribu? Wasaidie watoto kufikiria njia wanazoweza kumweka Mwokozi na mafundisho Yake ya kutia moyo “katika akili [yao] milele.”

Moroni 7:45–48

“Hisani ni upendo msafi wa Kristo.”

Kukuza karama ya hisani ni lengo la maisha yote. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwapa msukumo watoto kutafuta upendo msafi wa Kristo?

Shughuli za Yakini

  • Waalike watoto kushiriki kile wanachofikiri neno “hisani” humaanisha. Kisha mwalike mmoja wa watoto kusoma Moroni 7:45. (Ikiwa baadhi ya maneno katika mstari huu ni magumu kueleweka, wasaidie watoto kuyatafuta kwenye kamusi.) Waombe watoto wazungumze kuhusu watu wanaowafahamu ambao ni mifano mizuri ya hisani. Kwa nini hisani huitwa “upendo msafi wa Kristo”? (Moroni 7:47). Ni nini mstari wa 48 hutufundisha kuhusu jinsi tunavyoweza kujazwa na hisani? Muhimize kila mtoto kuomba kwa ajili ya hisani wiki hii na kutafuta njia za kuonyesha hisani kwa wengine.

  • Wasaidie watoto kufikiria njia ambazo Yesu alionyesha hisani (ona, kwa mfano, Luka 23:34; Yohana 8:1–11; Etheri 12:33–34). Je, ni kwa jinsi gani sisi tunaweza kufuata mfano Wake?

  • Waombe watoto waandike majina ya watu wanaowafahamu kwenye vipande vya karatasi na kuviweka kwenye mkoba au chombo kidogo. Waalike kwenda na chombo chao nyumbani, kuchagua jina kutoka kwenye chombo kila siku, na kufanya kitu kinachoonyesha upendo kwa mtu yule. Katika somo lijalo, waalike kushiriki uzoefu wao wa kuwatumikia watu hawa.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wahimize watoto kufikiria mtu ambaye anaweza kuwa anatafuta imani kubwa au tumaini katika Yesu Kristo. Waalike watoto kushiriki na mtu huyo jambo walilojifunza darasani leo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Himiza staha. Kipengele muhimu cha staha ni kufikiria juu ya Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Unaweza kuwakumbusha watoto kuwa wenye staha kwa kuimba kimya kimya au kwa mvumo au kuonyesha picha ya Yesu.

Chapisha