Mafundisho na Maagano 2021
Aprili 5–11. Mafundisho na Maagano 30–36: “Umeitwa Kuhubiri Injili Yangu”


“Aprili 5–11. Mafundisho na Maagano 30–36: ‘Umeitwa Kuhubiri Injili Yangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Aprili 5–11. Mafundisho na Maagano 30–36,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2021

Picha
wamisionari wa awali wa Kanisa

Aprili 5–11

Mafundisho na Maagano 30–36

“Umeitwa Kuhubiri Injili Yangu”

Unaposoma kwa sala Mafundisho na Maagano 30–36 pamoja na watoto wa darasa lako akilini, Roho anaweza kukupa mawazo kuhusu jinsi ya kuwafundisha. Tafuta mawazo ya ziada katika muhtasari huu.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Nyanyua juu picha ya wamisionari, na waombe watoto washiriki kile wanachofahamu kuhusu kazi ya umisionari.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mafundisho na Maagano 33:2–3, 6–10

Ninaweza kushiriki injili ya Yesu Kristo.

Hata watoto wadogo wanaweza kushiriki ushahidi wao wa injili ya Yesu Kristo. Ni kwa jinsi gani unaweza kutumia mistari hii ili kuwatia moyo wa kufanya hivyo?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wajaribu kusema kirai kama “Mungu anakupenda” vinywa vyao vikiwa vimefumbwa. Onesha kwamba hatuwezi kuwafundisha watu kuhusu injili kama hatufumbui vinywa vyetu. Soma Mafundisho na Maagano 33:8–10, na waalike watoto kufumbua vinywa vyao kila mara wanaposikia kirai “fumbueni vinywa vyenu.” Kwa nini Baba wa Mbinguni anatutaka tufumbue vinywa vyetu na kushiriki injili pamoja na wengine?

  • Wanong’oneze jambo watoto kwa utulivu, kama vile “Joseph Smith alikuwa Nabii wa Mungu,” na waombe warudie kile ulichosema. Kisha tamka kirai hicho hicho kwa sauti ya juu. Soma Mafundisho na Maagano 33:2. Wasaidie watoto kuelewa kwamba “kupaza sauti [zetu]” humaanisha kutokuwa waoga kuwaambia wengine kuhusu Yesu Kristo, Kitabu cha Mormoni, na kweli zingine za injili.

  • Weka wanasesere wa karatasi au picha za watu kuzunguka chumba. Waalike watoto kutafuta watu na kuwakusanya mbele ya darasa. Soma Mafundisho na Maagano 33:6, na uelezee kile inachomaanisha kwamba Bwana “atawakusanya wateule [Wake].” Shuhudia kwamba tunaweza kusaidia kuwakusanya watu kwa Bwana pale tunaposhiriki injili.

  • Imbeni wimbo kuhusu kushiriki injili, kama vile “I Want to Be a Missionary Now” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 168). Wasaidie watoto kufikiria jinsi wanavyoweza kuwasaidia watu wengine kujifunza kuhusu Yesu Kristo.

Mafundisho na Maagano 33:12–17

Ninaweza kuyajenga maisha yangu juu ya injili ya Yesu Kristo.

Ushauri alioutoa Bwana kwa Ezra Thayer na Northrop Sweet unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kujenga maisha yao juu ya injili ya Yesu Kristo.

Shughuli Yamkini

  • Waoneshe watoto picha ya msingi wa jengo, na waombe wauelezee. Kwa nini jengo linahitaji msingi imara, madhubuti? Soma pamoja na watoto Mafundisho na Maagano 33:12–13, na uelezee kwamba Bwana anatutaka tujenge maisha yetu juu ya injili Yake. Wasaidie watoto kufikiria baadhi ya njia wanazoweza kujenga maisha yao juu ya injili ya Yesu Kristo.

  • Wape watoto vitu kadhaa ambavyo wanaweza kutumia kujenga mnara, kama vile matofali au vikombe vya plastiki. Wekea alama kila kitu kwa picha inayowakilisha mambo ambayo Bwana alisema katika Mafundisho na Maagano 33:14–17. Waalike watoto kujenga mnara wakati unapozungumza nao kuhusu jinsi mambo haya yanavyotusaidia kujenga maisha yetu juu ya injili ya Yesu Kristo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mafundisho na Maagano 30:1–2

Ninapaswa kufokasi zaidi kwenye mambo ya Mungu kuliko mambo ya dunia.

Ushauri wa Bwana kwa David Whitmer katika sehemu ya 30 unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kubaki waaminifu kwenye injili ya Yesu Kristo.

Shughuli Yamkini

  • Someni Mafundisho na Maagano 30:1 pamoja, na waombe watoto wafanyie ufupisho, kwa maneno yao wenyewe, ushauri ambao Bwana alimpa David Whitmer. Ni kwa njia zipi wakati mwingine “tunamwogopa mwanadamu,” au kuhofia kile wengine wanachoweza kufikiria, badala ya kufanya kile tunachojua tunapaswa kufanya?

  • Waombe watoto wajaribu kufanya majukumu mawili kwa wakati mmoja, kama vile kukariri makala ya imani wakati wakiandika majina ya watoto wote darasani. Waulize kwa nini ilikuwa vigumu kufokasi kwenye jukumu la kwanza. Ni yapi baadhi ya “mambo ya dunia” (Mafundisho na Maagano 30:2) ambayo yanaweza kutuvuruga kutoka kwenye kumkumbuka Yesu Kristo na injili Yake? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuweka fokasi yetu Kwake badala ya kwenye mambo yenye umuhimu mdogo?

Mafundisho na Maagano 30–34

Ninaweza kushiriki injili ya Yesu Kristo.

Watoto wengi ndani ya Kanisa wanatazamia kutumikia misheni ya muda wote au misheni ya huduma. Uzoefu wa wamisionari uliozungumziwa katika sehemu za 30–34 ungeweza kuwasaidia kujitayarisha.

Shughuli Yamkini

  • Mualike mshiriki wa kata ajifunze kuhusu mmoja wa wamisionari aliyeitwa katika Mafundisho na Maagano 30–34 na kushiriki pamoja na watoto kile walichojifunza (ona “Sauti za Urejesho: Waongofu wa Mwanzo” katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia au “The Faith and Fall of Thomas Marsh,” “Ezra Thayer: From Skeptic to Believer,” “Orson Pratt’s Call to Serve,” Revelations in Context, 54–69).

  • Chora mdomo mkubwa ubaoni, na wasaidie watoto kutafuta katika Mafundisho na Maagano 33:8–10 ahadi za Bwana kwetu wakati tunapofumbua vinywa vyetu kushiriki injili. Waruhusu watoto waandike ahadi hizi ubaoni, na wasaidie kuelewa kile ahadi hizi zinachomaanisha. Muombe kila mtoto kuandika ndani ya mdomo ukweli wa injili wanaoweza kuushiriki pamoja na wengine.

  • Onesha picha ya tarumbeta, na zungumzia kuhusu kile inachomaanisha kuhubiri injili “kama kwa sauti ya tarumbeta.” Ni kwa jinsi gani “tunapaza” sauti zetu? (Mafundisho na Maagano 33:2; 34:6.

  • Waombe watoto washiriki jinsi wanavyojiandaa kutumikia misheni siku moja. Ikiwa wanamfahamu mtu (pengine mwanafamilia) ambaye anatumikia, waalike waeleze kuhusu uzoefu wake. Au waalike wamisionari, mmsionari aliyemaliza kutumikia, au mtu anayejiandaa kwa ajili ya misheni kushiriki shauku yake ya kazi ya umisionari. Shiriki baadhi ya uzoefu wako wa kushiriki injili, ikiwemo uzoefu katika maisha yako ya kila siku.

    Picha
    wavulana wakicheza

    Ninaweza kushiriki injili pamoja na rafiki zangu.

Mafundisho na Maagano 33:12–17

Ninaweza kuyajenga maisha yangu juu ya injili ya Yesu Kristo.

Ikiwa watoto watajifunza katika umri mdogo jinsi ya kuyajenga maisha yao juu ya injili ya Yesu Kristo, kuna uwezekano mkubwa wakabaki waaminifu Kwake. Ushauri uliotolewa katika mistari hii unaweza kuwasaidia.

Shughuli Yamkini

  • Leta darasani vitu vyenye ugumu tofauti, kama vile mnyama aliyejazwa makorokoro, sponji, udongo, na mwamba. Waruhusu watoto kubeba kila kimoja. Waombe kutafuta katika Mafundisho na Maagano 33:12–13 ili kupata jinsi Bwana anavyoelezea injili Yake. Kwa nini “mwamba” ni neno zuri la kuielezea injili? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuyajenga maisha yetu juu ya mwamba wa injili?

  • Wasaidie watoto kusoma Mafundisho na Maagano 33:12–17 na kutafuta mambo tunayoweza kufanya ili kuyajenga maisha yetu juu ya injili ya Yesu Kristo. Waalike watoto kuchora picha ya jambo wanalolipata, na waruhusu wabahatishe kile picha ya kila mmoja inachoelezea.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kuwa kama wamisionari kwa kushiriki pamoja na familia zao jambo walilojifunza katika Msingi leo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Shuhudia juu ya baraka zilizoahidiwa. Wakati unapowaalika watoto kuishi kanuni ya injili, shiriki ahadi ambazo Mungu amezitoa kwa wale wanaoishi kanuni hiyo. Kwa mfano, unaweza kutoa ushuhuda wa baraka ambazo Bwana hutoa kwa wale wanaofumbua vinywa vyao na kushiriki injili.

Chapisha