Mafundisho na Maagano 2021
Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66: “Bwana Anahitaji Moyo na Akili Yenye Kukubali.”


“Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66 : ‘Bwana Anahitaji Moyo na Akili Yenye Kukubali,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2021

Picha
Shamba wakati wa mapambazuko

Wilaya ya Jackson, Missouri

Juni 14–20

Mafundisho na Maagano 64–66

“Bwana Anahitaji Moyo na Akili Yenye Kukubali.”

Unapojiandaa kufundisha, fikiria jinsi unavyopaswa kubadili mtazamo wako ufae mahitaji ya watoto. Kumbuka kwamba unaweza kutumia shughuli yoyote katika muhtasari huu kwa ajili ya watoto wadogo au wakubwa.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Mpe kila mtoto nafasi ya kushika picha ya Mwokozi na kushiriki kitu fulani wanachojifunza kumhusu Yeye na injili Yake.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mafundisho na Maagano 64:9–10

Yesu Kristo anataka mimi nisamehe wengine.

Ni somo gani la vitendo au shughuli unayoweza kufikiria ambayo itawasaidia watoto kuelewa inamaanisha nini kusamehe? Unapojadili msamaha, wakumbushe watoto kwamba kusamehe hakumaanishi kuruhusu wengine watuumize.

Shughuli Yamkini

  • Soma kirai “mnapaswa kusameheana ninyi kwa ninyi” (Mafundisho na Maagano 64:9), na waulize watoto inamaanisha nini kumsamehe mtu fulani. Ili kuwasaidia kuelewa, shiriki mifano michache ya kawaida. Wasaidie kuigiza mifano hii ili kufanya mazoezi ya kusamehe.

  • Soma Mafundisho na Maagano 64:10 pole pole kwa watoto, na watake kushikana mikono na mtoto mwingine wanaposikia neno “samehe.” Shiriki ushuhuda wako wa amani na furaha ambao unakuja tunaposamehe wengine.

  • Imbeni wimbo kuhusu msamaha, kama vile “Help Me, Dear Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99). Wimbo huu unatufundisha nini kuhusu kusamehe wengine?

Mafundisho na Maagano 64:34

Ninaweza kumtii Yesu kwa moyo na akili yangu.

Bwana aliwafundisha Watakatifu kwamba kujenga Sayuni, walihitaji kumpa Yeye mioyo yao na akili zilizo tayari. Fikiria jinsi utakavyoweza kuwasaidia watoto kuanza kufikiria hii ina maana gani kwao.

Shughuli Yamkini

  • Soma kwa watoto kutoka Mafundisho na Maagani 6434: “Tazama, Bwana anahitaji moyo na akili yenye kukubali.” Rudia kifungu hiki cha maneno mara chache, ukionyesha kwenye moyo wako na kichwa unaposoma maneno hayo, na watake watoto kufanya hivyo hivyo. Jinsi gani tunaweza kutoa mioyo na akili zetu kwa Mwokozi? (Inaweza kusaidia kuelezea kwamba moyo wetu unahusu hisia zetu na upendo na akili zetu zinahusu mawazo yetu.)

  • Imbeni wimbo kuhusu kumpenda na kumfuata Mwokozi kama vile “I Feel My Savior’s Love” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 74–75); hususani mstari wa 3). Tunamwonyeshaje Mwokozi kwamba tunampenda? Shiriki hisia zako kwa ajili ya Yesu Kristo.

Mafundisho na Maagano 66

Bwana anajua mimi ni nani na ananipenda.

William E.McLellin alikuwa na maswali matano mahususi kwa Bwana. Joseph Smith alipokea majibu yake katika ufunuo japokuwa hakujua maswali ya William yalikuwa nini. Uzoefu huu ungeweza kukusaidia wewe kufundisha watoto kwamba Mungu anawafahamu na anaweza kujibu maswali yao.

Shughuli Yamkini

  • Simulia kuhusu jinsi Bwana alivyojibu maswali ya William E. McLellin kupitia ufunuo kutoka kwa Nabii Joseph Smith (ona Mafundisho na Maagano 66, kichwa cha habari cha sehemu). Shuhudia kwamba Baba wa Mbinguni anatujua sisi na anataka kutusaidia. Waombe watoto kushiriki jinsi wanavyojua kwamba Mungu anawapenda.

  • Wasomee watoto Mafundisho na Maagano 66:4. Waeleze watoto kuhusu muda Bwana alipokuonyesha nini alitaka wewe ufanye. Soma mstari tena, wakati huu ingiza jina la mmoja wa watoto. Rudia kwa ajili ya kila mtoto.

    Picha
    Yesu na watoto

    Yesu Kristo anampenda kila mmoja wetu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mafundisho na Maagano 64:7–10

Bwana ananitaka nisamehe kila mtu.

Kama mistari hii inavyoonyesha, hata wafuasi wa Yesu Kristo wakati mwingine walikuwa na tatizo kusameheana. Fikiria jinsi utakavyoweza kuwasaidia watoto kuelewa amri ya Mungu ya “kusamehe wote.” (Weka wazi kwamba kusamehe haimaanishi kuruhusu watu kutuumiza; wanapaswa siku zote kumweleza mtu mzima anayeaminika kama mtu fulani anawaumiza.)

Shughuli Yamkini

  • Watake watoto kufikiria kwamba walitakiwa kumfundisha ndugu yao mdogo kuhusu kuwasamehe wengine. Wangefanya vipi? Waalike watoto wasome Mafundisho na Maagano 64:7–10 wawili wawili na kutafuta virai watakavyotumia katika mafundisho yao. Wangeweza pia kufanya mazoezi kufundishana wao kwa wao.

  • Imbeni pamoja “Help Me, Dear Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99). Jinsi gani Baba wa Mbinguni anatusaidia kusamehe wengine?

  • Fikiria analojia ambayo inaweza kusaidia watoto kuelewa jinsi “tunavyoteseka” wakati hatusamehi (mstari wa 8). Kwa mfano, waonyeshe watoto mfuko wa matope au uchafu; watake wafikirie kwamba mtu fulani aliwamwagia tope. Jinsi gani kushindwa kusamehe ni kama kutunza matope na siku zote kuyabeba pamoja nasi? Kwa nini itakuwa vyema zaidi kuyatupa matope mbali? Wasaidie watoto kufikiria analojia zingine ambazo hufundisha kwa nini ni muhimu kusamehe.

Mafundisho na Maagano 64:33–34

Bwana anahitaji “moyo wangu na akili yenye kukubali.”

Kujenga Sayuni—au kusaidia Kanisa kukua—ni “kazi kubwa.” Kuikamilisha, Bwana anatuhitaji kumpa mioyo yetu na akili zenye kukubali. Hao wanaoishi Sayuni ni “wa moyo mmoja na wazo moja” (Musa 7:18).

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto baadhi ya vitu ambavyo vimetengenezwa na sehemu ndogo ndogo nyingi, kama fumbo au zulia. Wasaidie kufikiria mifano mingine. Waalike watoto wasome Mafundisho na Maagano 64:33. Mungu anataka sisi tufanye nini ili kumsaidia kukamilisha “kazi Yake kubwa”? Je, ni “vitu gani vidogo” tunavyoweza kufanya ambavyo vitasaidia kukamilisha kazi hii?

  • Watake watoto kukamilisha kitendo ambacho kinahitaji vitu viwili, lakini wape kimoja tu (kwa mfano, andika ubaoni bila chaki au kukata kipande cha karatasi bila mkasi). Watake watoto wasome Mafundisho na Maagano 64:34 kutafuta ni vitu gani viwili Bwana anavitaka kutoka kwetu. Kwa nini tunahitaji kutoa vyote moyo wetu na akili kwa Bwana? Jinsi gani tutafanya hili?

Mafundisho na Maagano 65

Ninaweza kusaidia kuuandaa ulimwengu kumpokea Yesu Kristo.

Misheni ya Kanisa—ufalme wa Mungu duniani—ni kuuandaa ulimwengu kwa ajili ya kurudi kwa Mwokozi. Watoto unaowafundisha ni sehemu muhimu ya misheni hii. Unaweza kufanya nini kuwasaidia washiriki?

Shughuli Yamkini

  • Kama darasa au wawili wawili, soma Mafundisho na Maagano 65, na hesabu mara ngapi neno “andaa” limeandikwa. Bwana anatutaka sisi tujiandae kwa ajili gani? Tunaweza kufanya nini ili kujiandaa wenyewe na kuiandaa dunia?

  • Onyesha picha ya Ujio wa Pili wa Mwokozi (ona Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 66), na waombe watoto waelezee kile wanachokiona au kile wanachokijua kuhusu tukio hili. Wape watoto maneno muhimu na vifungu vya maneno kuvitafuta katika Mafundisho na Maagano 65 (kama vile “ilijaza ulimwengu wote” na “kazi za ajabu”). Maneno haya na vifungu vya maneno vinatufundisha nini kuhusu Ujio wa Pili na jukumu letu katika kujiandaa kwa ajili ya hilo?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wasaidie watoto kutafuta mstari katika Mafundisho na Maagano 64–66 ambao wanapenda na wangependa kutaka kuushiriki pamoja na mwanafamilia au rafiki.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Jifunze kutambua ufunuo. Unapoomba na kutafakari kuhusu maandiko, utaona kwamba mawazo na misukumo vinaweza kuja wakati wowote na sehemu yoyote—“unapokwenda kazini, kufanya kazi za nyumbani, au kuingiliana na familia na marafiki” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,12).

Chapisha