Mafundisho na Maagano 2021
Desemba 13–19. Familia: Tangazo kwa Ulimwengu: “Familia Ni Kitovu cha Mpango wa Muumbaji”


“Desemba 13–19. Familia: Tangazo kwa Ulimwengu: ‘Familia Ni Kitovu cha Mpango wa Muumbaji,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Desemba 13–19. Familia: Tangazo kwa Ulimwengu,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2021

Picha
familia

Desemba 13–19

Familia: Tangazo kwa Ulimwengu

“Familia Ni Kitovu cha Mpango wa Muumbaji”

Je, ni kanuni gani unazipata katika “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu” ambazo unahisi mwongozo wa kiungu kuzishiriki na watoto? Unapojiandaa kufundisha, andika ushawishi uliopokea kutoka kwa Roho.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto kuleta au kuchora picha za familia zao ili wazioneshe kwa darasa. Waombe watoto kushiriki kitu ambacho wao wanakipenda kuhusu familia zao au kile walichojifunza kuhusu familia wiki hii.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Familia ni muhimu katika mpango wa Baba wa Mbinguni.

Je, unawezaje kutumia tangazo la familia ili kuwasaidia watoto kuelewa jinsi familia zilivyo muhimu katika mpango wa Mungu?

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kufikiria juu ya mambo ambayo ni muhimu sana kwamba wangetaka kumwambia kila mtu kuhusu hayo. Waoneshe watoto nakala ya “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu,” na eleza kwamba manabii na mitume waliliandika hilo ili kumwambia kila mtu jinsi familia zilivyo muhimu kwa Baba wa Mbinguni. Waulize watoto kwa nini wanafikiri familia ni muhimu sana kwa Baba wa Mbinguni. Shiriki kitu kutoka kwenye tangazo ambacho unahisi kila mtu anahitaji kukijua.

  • Waoneshe watoto picha ya hekalu na picha ya familia. Acha watoto washikilie hizo picha wakati wewe unasoma sentensi ya mwisho ya aya ya tatu ya tangazo la familia. Waombe watoto kuonesha kwa kidole picha sahihi wakati unaposoma maneno “mahekalu” na “familia.” Toa ushuhuda kwamba kwa sababu ya ibada za hekaluni, familia zetu zinaweza kuungana milele. Imbeni pamoja wimbo kuhusu familia za milele, kama vile “I Love to See the Temple” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 95), na wasaidie watoto kusikiliza maneno kama “hekalu” na “familia.”

  • Waulize watoto kile wanachoweza kufanya ili kufanya vitu kadhaa kuwa imara—kama vile meno, miili yetu, au majengo. Tunaweza kufanya nini ili kuzifanya familia zetu ziwe imara? Wasaidie watoto kuelewa kanuni ambazo hutuongoza kwenye furaha katika maisha ya familia, zipatikanazo katika aya ya saba ya tangazo la familia (ona pia ukurasa wa shughuli ya wiki hii). Wasaidie watoto kupanga njia watakazotumia kuimarisha familia zao.

    Picha
    familia ikipika

    Wazazi wanapaswa kuwalea watoto wao kwa upendo na uadilifu.

Mimi ni “mwana au binti mpendwa wa kiroho wa wazazi wa mbinguni.”

Tangazo la familia linafundisha kwamba sisi sote ni watoto wa Wazazi wa Mbinguni na tuko hapa duniani ili tuwe zaidi kama Wao.

Shughuli Yamkini

  • Imbeni pamoja “I Am a Child of God” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 2–3). Kisha rusha mpira au kitu laini kwa mtoto wakati ukisema, “ninamjua mtoto wa Mungu anayeitwa [jina la mtoto].” Mwombe mtoto kurusha kitu hicho kwa mtoto mwingine, akisema maneno yale yale na kuingiza jina la mtoto anayemrushia. Rudia shughuli hii mpaka kila mmoja apate zamu. Shuhudia kwamba kila mtoto ni “mwana au binti mpendwa wa kiroho wa wazazi wa mbinguni.”

  • Fikiria njia unazoweza kuonesha kwamba kwa sababu sisi ni watoto wa Wazazi wa Mbinguni, tunaweza kuwa kama Wao. Kwa mfano, onesha picha za wanyama na watoto wao, au ya kwako na wazazi wako au watoto wako, na wasaidie watoto kuona mfanano. Toa ushuhuda kwamba kama vile ambavyo watoto hukua na kuwa kama wazazi wao, sisi tunaweza siku moja kuwa kama Wazazi wetu wa Mbinguni.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Familia ni kitovu cha Mpango wa Baba wa Mbinguni.

Tangazo la familia lilitolewa ili kuthibitisha upya kweli kuhusu familia. Fikiria jinsi utakavyowasaidia watoto kukuza shuhuda zao juu ya kweli hizi.

Shughuli Yamkini

  • Waulize watoto kama wanajua nani aliandika tangazo la familia. (Katika ujumbe wake “Mpango na Tangazo” [Ensign au Liahona, Nov. 2017, 28–31], Rais Dallin H. Oaks alielezea jinsi lilivyoandikwa.) Wasaidie watoto kuelewa maneno “kwa dhati tunatangaza” katika aya ya kwanza yanamaanisha nini. Waombe kushiriki mawazo yao kuhusu kwa nini manabii na mitume wanataka “kwa dhati kutangaza” kweli kuhusu familia katika siku yetu.

  • Shiriki kauli chache kutoka tangazo la familia ambazo ni za maana sana kwako. Waalike watoto kuelezea hisia zao kuhusu kweli hizo. Je, ni kwa jinsi gani maisha yetu yangekuwa tofauti kama tusingejua mambo haya? Imbeni pamoja wimbo ambao unahusiana na kweli zinazopatikana katika tangazo, kama vile “I Will Follow God’s Plan” au “Families Can Be Together Forever” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 164–65, 188).

  • Waoneshe watoto picha (au waalike kuchora) zinazoonesha kweli zinazopatikana katika tangazo la familia. Hizi zinaweza kuwa picha za hekalu, familia ikisali, au kucheza pamoja, au wanandoa wakifunga ndoa. Waalike watoto kutafuta sentensi katika tangazo la familia ambazo zinahusiana na picha hizo. Je sentensi hizi zinatufundisha nini?

  • Andaa maswali ambayo yanaweza kujibiwa katika tangazo la familia, kama vile “Je, Mungu anahisi nini kuhusu ndoa?” na “Kitu gani hutengeneza familia yenye furaha?” Acha kila mtoto achukue swali, na wasaidie kutafuta majibu katika tangazo.

  • Mwalike mama na baba wa mmoja wa watoto ili washiriki na darasa jinsi wao “wanavyosaidiana kama wenza sawa” katika “majukumu yao matakatifu” katika familia yao. Waalike watoto kujadiliana kile wanachoweza kufanya sasa ili wajitayarishe kuwa wake na waume, mama na baba waadilifu.

Familia zina furaha zaidi pale wanapomfuata Yesu Kristo.

Baba wa Mbinguni anampenda kila mmoja wa watoto wake, na anataka wawe na furaha. Je, unawezaje kuwasaidia watoto unaowafundisha kuelewa kwamba furaha ya kweli huja kutokana na kufuata mafundisho na mfano wa Mwokozi wetu Yesu Kristo?

Shughuli Yamkini

  • Chora picha kubwa ya moyo ubaoni, na waalike watoto kusoma aya ya saba ya tangazo. Waombe watafute mambo wanayoweza kufanya ili kusaidia familia zao kuwa na furaha, na kuandika majibu yao ndani ya moyo huo. Waalike watoto kuchagua kitu fulani ambacho wataanza kukifanyia kazi ili kufanya nyumba zao kuwa na furaha zaidi.

  • Waalike watoto kushiriki uzoefu wao wakati walipohisi kupendwa na mwanafamilia. Wasaidie watoto kutambua kanuni kutoka katika aya ya saba ya tangazo ambayo inaweza kuwasaidia wanafamilia kujisikia kupendwa. Je, ni kwa namna gani uelewa wetu juu ya injili ya Yesu Kristo unaathiri namna tunavyowatendea wanafamilia wetu?

  • Waulize watoto ni nini wangesema kama rafiki angewauliza wao kwa nini kuoa au kuolewa au kuwa na watoto ni muhimu. Je, tungewezaje kumsaidia rafiki huyu kuelewa jinsi familia zilivyo muhimu kwa Baba wa Mbinguni? Wasaidie watoto kutafuta maelezo katika tangazo la familia ambayo yangeweza kuwasaidia; ona pia video ya “What Is the Purpose of Family?” (ChurchofJesusChrist.org).

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kutengeneza mpango wa kufanya kitu fulani ili kuimarisha familia zao. Wahimize kushiriki mipango yao kwa wanafamilia wao nyumbani.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kuwa makini. Unapofundisha kweli zilizofundishwa katika tangazo la familia, tafadhali tambua kwamba watoto wengi wanalelewa katika familia ambazo hazifanani na maadili yaliyoelezwa katika tangazo hili. Kuwa mwangalifu usije sema kitu chochote ambacho kinaweza kuwafanya wahisi kukata tamaa au kuwa wanyonge

Chapisha