Mafundisho na Maagano 2021
Desemba 20–26. Krismasi: Zawadi Isiyo na Mfano ya Mwana Mtukufu wa Mungu


“Desemba 20–26. Krismasi: Zawadi Isiyo na Mfano ya Mwana Mtukufu wa Mungu,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Desemba 20–26. Krismasi,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2021

Picha
sanaa ya Mariamu na mtoto Yesu

Siku ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo katika Shaba na Kijani Kibichi, na J. Kirk Richards

Desemba 20–26

Krismasi

Zawadi Isiyo na Mfano ya Mwana Mtukufu wa Mungu

Krismasi ni wakati wa kusisimua kwa watoto wengi. Fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia kuunganisha shangwe ya wakati wa Krismasi na shangwe ya injili ya Mwokozi.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waombe watoto kueleza kile walichofanya wiki iliyopita ili kusherehekea kuzaliwa kwa Mwokozi.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Ninaweza “kutoa ushuhuda [wangu]” ili kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu.

Katika “Kristo Aliye Hai” (ChurchofJesusChrist.org), Urais wa Kwanza na Akidi ya Mitume Kumi na Wawili wametoa ushuhuda wao juu ya Yesu Kristo ili “kuadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo.” Fikiria jinsi utakavyowatia moyo watoto kutoa shuhuda zao kwa wengine.

Shughuli Yamkini

  • Waoneshe watoto nakala ya “Kristo Aliye Hai” (ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia). Onesha kwa kidole neno Kristo katika kichwa cha habari, na acha watoto nao waoneshe vile vile. Na pia onesha kwa kidole saini chini ya ukurasa, na waambie watoto kwamba katika mwaka 2000, Urais wa Kwanza na Mitume Kumi na Wawili waliandika ushuhuda wao juu ya Yesu Kristo, wakatia saini kwa majina yao, na kuushiriki na ulimwengu.

  • Onesha picha ya Yesu Kristo, na mwalike kila mtoto kusimama na kushiriki kitu anachokijua kuhusu Yeye. Kama wanahitaji msaada, pendekeza kweli kutoka “Kristo Aliye Hai.” Wakumbushe watoto kwamba wanapowaambia wengine kuhusu Yesu, wanashiriki na wengine shuhuda zao.

  • Waambie watoto jinsi wewe ulivyopata ushuhuda wako juu ya Yesu Kristo na kile unachofanya ili kuutunza ushuhuda wako uwe imara. Wasaidie kufikiria njia wanazoweza kuimarisha shuhuda zao juu ya Yesu Kristo, na waalike kuchagua jambo moja watakalofanya.

Baba wa Mbinguni alimtuma Mwanawe kama zawadi kwetu sisi.

Kutoa na kupokea zawadi ni sehemu ya desturi ya Krismasi kwa watu wengi. Desturi hii inapaswa kutusaidia sisi kukumbuka “zawadi isiyo na mfano ya Mwana Mtukufu wa Mungu” (“Kristo Aliye Hai”).

Shughuli Yamkini

  • Waombe watoto waeleze kuhusu zawadi walizotoa au kupokea. Wasomee sentensi ya mwisho ya “Kristo Aliye Hai,” na waalike kusikiliza juu ya zawadi Mungu aliyotupatia sisi. (Kama itahitajika, wasaidie kuelewa kwamba “isiyo na mfano” maana yake ni “bora kuliko nyingine yoyote.”) Je, kwa nini Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ni zawadi bora zaidi?

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu Yesu Kristo, kama vile “He Sent His Son” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 34–35). Wasaidie watoto kuchukua kifungu cha maneno kutoka kwenye wimbo ambacho wangependa kuchora (kama vile “mtoto mchanga” au “kutembea na watu”). Wanapochora, waombe watoto wakuambie jinsi wanavyohisi kuhusu yale ambayo Yesu amefanya kwa ajili yao. Na wewe vile vile shiriki hisia zako.

Yesu Kristo ananialika kufuata mfano Wake.

Sehemu ya “ushawishi … mkubwa sana” wa Mwokozi juu ya ulimwengu umekuwa ni mfano Wake mkamilifu. Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwahamasisha watoto kumfuata Yeye?

Shughuli Yamkini

  • Kutoka katika aya ya pili ya “Kristo Aliye Hai,” wasomee watoto baadhi ya mambo ambayo Yesu alifanya. Onesha picha za maisha Yake (ona ukurasa wa shughuli ya wiki hii), na waalike watoto kuzungumzia kuhusu kile Mwokozi anachofanya katika picha hizo. Wasaidie kufikiria njia wanazoweza kufuata mfano Wake.

  • Chagua video ya “Light the World” (ComeuntoChrist.org) kuwaonesha watoto, au waambie wakati ambapo wewe ulibarikiwa kwa huduma kama ya Kristo iliyofanywa na mtu fulani. Mwalike mtoto kufanya tendo rahisi la huduma, na waombe watoto wengine kubahatisha kile mtoto huyo anachofanya. Acha kila mtoto apate zamu. Wasaidie watoto kufikiri juu ya kitu wanachoweza kufanya ili kumtumikia mtu fulani katika familia zao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

“Tunatoa shuhuda zetu.”

Mfano wa manabii na mitume walioandika “Kristo Aliye Hai” unaweza kuwahamasisha watoto kutoa shuhuda zao juu ya Yesu Kristo.

Shughuli Yamkini

  • Andika ubaoni Ninajua kwamba Yesu Kristo … na waalike watoto kuelezea njia za kumalizia sentensi hii. Pendekeza kwamba waangalie katika “Kristo Aliye Hai” kupata mawazo. Tunaweza kufanya nini ili kuimarisha shuhuda zetu juu ya Yesu Kristo? Je, wengine wanabarikiwaje wakati sisi tunapotoa shuhuda zetu?

  • Eleza kwamba “Kristo Aliye Hai” ilisainiwa na Urais wa Kwanza na Mitume Kumi na Wawili. Someni pamoja Mafundisho na Maagano 107:23. Je, ni kitu gani kinawafanya Mitume kuwa tofauti “na maafisa wengine katika kanisa”? Chagua moja ya video za “Special Witnesses of Christ” ili kuangalia pamoja na watoto (ChurchofJesusChrist.org). Je, ni kwa nini tunashukuru kuwa na mashahidi maalumu wa Kristo katika siku yetu?

“Hakuna mwingine aliyewahi kuwa na ushawishi mkubwa kama huu”

Katika “Kristo Aliye Hai,” manabii na mitume wametamka kuwa hakuna mtu aliyewahi kuwa na ushawishi mkubwa kwa watoto wa Mungu kuliko Yesu Kristo. Fikiria jinsi utakavyowasaidia watoto kujifunza kuhusu ushawishi mkubwa wa Mwokozi juu yetu sisi sote.

Shughuli Yamkini

  • Mpe kila mtoto kifungu cha maneno au sentensi kutoka “Kristo Aliye Hai,” na waombe wachore picha ya kifungu au sentensi hiyo. Kila mtoto anapoonesha kwa darasa picha yake, waombe watoto wengine kubahatisha ile picha inaonesha nini na tafuta mstari unaoshabihiana nayo katika “Kristo Aliye Hai.” Je, ni kwa jinsi gani sisi tunabarikiwa kwa sababu ya maisha na huduma ya Yesu Kristo?

  • Wasaidie watoto kutafuta majina au vyeo tofauti vya Yesu Kristo katika “Kristo Aliye Hai” na kupigia mstari, ikiwezekana (baadhi ya mifano inajumuisha Masiya, Mzaliwa wa Kwanza, mwanzo na mwisho, mtetezi, jiwe kuu la pembeni). Zungumza kuhusu kile ambacho kila moja ya vyeo hivi kinatufundisha kuhusu Yeye. (Baadhi ya vyeo hivi vimefafanuliwa katika Mwongozo kwenye Maandiko au Kamusi ya Biblia.)

Yeye ni nuru, uzima, na tumaini la ulimwengu.”

Krismasi ni majira ya shangwe kwa sababu ya tumaini ambalo Yesu Kristo amelileta ulimwenguni kupitia mafundisho, mfano na dhabihu Yake ya kulipia dhambi.

Picha
Yesu Kristo

Nuru ya Ulimwengu, na Howard Lyon

Shughuli Yamkini

  • Mualike kila mtoto kuchora mti wa Krismasi, au wewe uchore mmoja ubaoni. Waalike watoto waupambe mti huo kwa maneno au vifungu vya maneno kutoka katika “Kristo Aliye Hai” ambavyo vinaelezea zawadi ambazo Mwokozi ametupatia sisi (kama vile “nuru,” “uzima,” na “tumaini”). Acha wazungumze kuhusu kwa nini walichagua maneno au vifungu hivyo.

  • Wasaidie watoto kuchagua nyimbo za Krismasi ambazo hutuambia juu ya nuru, uzima, na tumaini ambavyo kuzaliwa kwa Mwokozi kumevileta ulimwenguni—kwa mfano, “O Little Town of Bethlehem” au “Hark! The Herald Angels Sing” (Nyimbo za Kanisa, na. 208–9). Imbeni nyimbo hizo pamoja, na acha watoto waelezee jinsi gani Kristo ameleta nuru, uzima, na tumaini katika maisha yao.

  • Waombe baadhi ya watoto kusoma kuhusu wachungaji katika Luka 2:8–20. Waombe wengine wasome kuhusu Simoni katika Luka 2:25–33. Waalike kuelezana wao kwa wao jinsi wachungaji na Simoni walivyojisikia walipogundua kwamba Yesu amezaliwa. Kwa nini walijisikia namna hii? Je, ni kwa nini kuzaliwa Kwake kunatuletea “shangwe kuu”?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kumfikiria mtu katika familia zao ambaye pamoja naye wanaweza kushiriki shuhuda zao juu ya Yesu Kristo. Wasaidie kufikiria kile ambacho wanaweza kusema ili kuimarisha imani ya mtu huyo kwa Kristo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Jitayarishe kwa kusoma maandiko. “Kusoma neno la Mungu kwa sala hutuweka sisi katika uwiano na Roho Mtakatifu. Kisha Yeye ataweza kutupa mwongozo wa kiungu kuleta kile tulichojifunza wakati tunapowafundisha na kuwainua wengine” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 12).

Chapisha