119 Mji Mwema, Bethlehemu Kwa utulivu 1. Mji mwema, Bethlehemu, Tuli watulia. Ulalapo, nyota nazo Zinapita kimya; Na gizani yang’aa Nuru ya milele. Tumaini za vizazi Zatimia nawe. 2. Hivyo Kristo azaliwa; Malaika juu Wakalinda kwa upendo Wakistaajabu. Nyota za alfajiri Ujio tangaza, Imbeni sifa kwa Mungu, Kwa watu faraja. 3. Kimyakimya, hivyo ndivyo Zawadi hupewa! Mungu atoa kwa watu Za kwake baraka. Hawataona aja; Ila duniani, Kote wapole walipo Kristo aja kweli. Maandishi: Phillips Brooks, 1835–1893 Muziki: Lewis H. Redner, 1831–1908 Mika 5:2 Luka 2:4–16