9 Lo! Mlimani Kumora Kwa kutafakari / Kwa ari 1. Malaika wa juu Kavunja kimya chake; Kashuka kwenye mbingu, Haya maneno yake: Lo! Mlimani Kumora Maandiko yamefichwa. Lo! Mlimani Kumora Maandiko yamefichwa. 2. Na kwa muda mrefu Alificha Moroni; Akingojea Mungu Aitolee amri. Itafunuliwa tena Kufanya njia ya Bwana. Itafuunuliwa tena Kufanya njia ya Bwana. 3. Inazungumzia Uzao wa Yusufu Na yale mataifa, Yaliyo mapotevu. Na utimilifu huo, Wa injili yake Kristo. Na utimilifu huo Wa injili yake Kristo. 4. Sasa ndiyo wakati, Uliotarajiwa; Ulimwengu utii, Giza litatoweka. Kitabu kifunguliwe, Duniani kiangaze. Kitabu kifunguliwe, Duniani kiangaze. 5. Tazama Israeli Watakusanywa kwao Watajenga kwa mali Yerusalemu yao, Na Sayuni itang’aa, Ukweli ikieneza. Na Sayuni itanga’a, Ukweli ikieneza. Maandishi: Parley P. Pratt, 1807–1857 Muziki: John E. Tullidge, 1806–1873 Joseph Smith—Historia ya 1:30–34 Mafundisho na Maagano 128:20