165 Maisha Yaliyo Mema Kwa kutafakari 1. Maisha yaliyo mema Huakisi wako wema; Unatubariki, Mungu, Kupitia ndugu zetu. 2. Ni zawadi gani kubwa, Ni zawadi gani bora, Kama walio na Yesu Kukuza imani zetu. 3. Na rafiki kama huyu, Mioyoni atadumu Kutukumbusha vizuri Kukaribia mbinguni. 4. Twakushukuru Mwokozi Kwa marafiki wazuri, Walio waaminifu, Na wanaokuabudu. Maandishi: Karen Lynn Davidson, 1943–2019. © 1985 IRI Muziki: A. Laurence Lyon, 1934–2006. © 1985 IRI Mithali 17:17 Mithali 4:18 Mafundisho na Maagano 42:45–46