95 Tunaposhiriki Nembo Kwa hamasa 1. Tunaposhiriki nembo Kwa jina la Yesu Kristo, Sote na tuihakiki Mioyo kama ni safi. 2. Kristo damu alimwaga, Golgotha ilimwagika, Kifungo kutunusuru Na kuepuka adhabu. 3. Hivyo Yesu alikufa Ili haki kutimia, Ili watu tuwe huru Na kifo pia kuzimu. 4. Lakini tutafufuka, Na tutaishi daima, Hatutateswa na kifo, Tutatawala na Kristo. Maandishi: John Nicholson, 1839–1909 Muziki: Alexander Schreiner, 1901–1987. © 1948 IRI Jina la tuni: AEOLIAN Mafundisho na Maagano 20:40 Alma 5:19, 21