104 Ona Mkombozi Afa Kwa unyenyekevu 1. Ona Mkombozi afa, Deni la haki kulipa. Afa dhabihu ya dhambi, Afa dhabihu ya dhambi, Ili tupate ushindi. 2. Mateso yake wabeza, Hata mbavu wamchoma; Kwa dharau na kebehi, Kwa dharau na kebehi, Miiba avikwa taji. 3. Akapatwa na mateso Hakunung’unika neno. Wajibu atekeleza, Wajibu atekeleza, Na Baba amtukuza. 4. “Baba, ondoa kikombe, Upendavyo, ndivyo iwe. Nimefanya kazi yako, Nimefanya kazi yako; Ipokee yangu Roho.” 5. Alikufa; kwa uchungu, Jua likaficha nuru! Na kwa huzuni, dunia, Na kwa huzuni, dunia Ikajibu, “Mungu afa!” 6. Aishi— aishi sasa, Mbele ya hizi ishara, Twaja kwa unyenyekevu, Twaja kwa unyenyekevu, Amri zake kuheshimu. Maandishi: Eliza R. Snow, 1804–1887 Muziki: George Careless, 1839–1932 Mafundisho na Maagano 18:11 Luka 22:42 Luka 23:46