121 Nilisikia Kengele Kwa kutafakari 1. Nilisikia kengele, Zikilia pande zote, Nyimbo zao za upendo: “Amani kwa watu wote.” 2. Niliwazia kengele Zililia siku ile Nyimbo nzuri za Krismasi: “Amani kwa watu wote.” 3. Nilihisi kufa moyo, Amani kutokuwepo, Dunia inakejeli: “Amani kwa watu wote.” 4. Nyimbo zikanikumbusha: Mungu yupo, hajalala, Haki itatushindia, “Amani kwa watu wote.” 5. Nyimbo ziliendelea, Usiku hadi mchana, Kwa sauti ya ahadi: “Amani kwa watu wote.” Maandishi: Henry Wadsworth Longfellow, 1807–1882 Muziki: John Baptiste Calkin, 1827–1905 Luka 2:14 Mafundisho na Maagano 3:1–3