Muziki
Baki Nami; Kumekuchwa


88

Baki Nami; Kumekuchwa

Kwa sala

1. Baki nami; kumekuchwa.

Muda ni jioni;

Giza sasa laingia;

Haliepukiki.

Moyoni mwangu, mwalikwa,

Kaa nami kwangu.

[Chorus]

Mwokozi baki na mimi;

Ona, kumekuchwa.

Mwokozi baki na mimi;

Ona, kumekuchwa.

2. Baki nami; kumekuchwa.

Kuwapo pamoja

Kumegusa moyo wangu,

Tulipoongea.

Umejaza nafsi yangu

Kwa kuwa karibu.

[Chorus]

Mwokozi baki na mimi;

Ona, kumekuchwa.

Mwokozi baki na mimi;

Ona, kumekuchwa.

3. Baki nami; kumekuchwa.

Usiku mpweke

Kama hutanena nami,

Uniangazie.

Giza, linanitishia,

Kuingia kwangu.

[Chorus]

Mwokozi baki na mimi;

Ona, kumekuchwa.

Mwokozi baki na mimi;

Ona, kumekuchwa.

Maandishi: M. Lowrie Hofford, 1823–1888

Muziki: Harrison Millard, 1830–1895

Luka 24:29 (13–32)

Chapisha