130
Kuna Nuru Moyoni Mwangu
Kwa furaha
1. Kuna nuru moyoni mwangu,
Ng’aavu tukufu,
Kuliko ya duniani.
Yesu mwanga wangu.
[Chorus]
Kuna nuru na baraka,
Siku inapokuwa nzuri,
Akitabasamu Yesu,
Kuna nuru moyoni.
2. Kuna wimbo moyoni mwangu,
Kumsifu Bwana,
Na anasikia wimbo
Usioimbika.
[Chorus]
Kuna nuru na baraka,
Siku inapokuwa nzuri,
Akitabasamu Yesu,
Kuna nuru moyoni.
3. Kuna upya moyoni mwangu,
Akiwepo Bwana,
Amani ipo rohoni,
Neema anipa.
[Chorus]
Kuna nuru na baraka,
Siku inapokuwa nzuri,
Akitabasamu Yesu,
Kuna nuru moyoni.
4. Kuna shangwe moyoni mwangu,
Sifa na shukrani
Kwa baraka zake Mungu,
Hapa na mbinguni.
[Chorus]
Kuna nuru na baraka,
Siku inapokuwa nzuri,
Akitabasamu Yesu,
Kuna nuru moyoni.
Maandishi: Eliza E. Hewitt, 1851–1920
Muziki: John R. Sweney, 1837–1899
Isaya 60:19
Zaburi 16:9, 11