Muziki
Kuna Nuru Moyoni Mwangu


130

Kuna Nuru Moyoni Mwangu

Kwa furaha

1. Kuna nuru moyoni mwangu,

Ng’aavu tukufu,

Kuliko ya duniani.

Yesu mwanga wangu.

[Chorus]

Kuna nuru na baraka,

Siku inapokuwa nzuri,

Akitabasamu Yesu,

Kuna nuru moyoni.

2. Kuna wimbo moyoni mwangu,

Kumsifu Bwana,

Na anasikia wimbo

Usioimbika.

[Chorus]

Kuna nuru na baraka,

Siku inapokuwa nzuri,

Akitabasamu Yesu,

Kuna nuru moyoni.

3. Kuna upya moyoni mwangu,

Akiwepo Bwana,

Amani ipo rohoni,

Neema anipa.

[Chorus]

Kuna nuru na baraka,

Siku inapokuwa nzuri,

Akitabasamu Yesu,

Kuna nuru moyoni.

4. Kuna shangwe moyoni mwangu,

Sifa na shukrani

Kwa baraka zake Mungu,

Hapa na mbinguni.

[Chorus]

Kuna nuru na baraka,

Siku inapokuwa nzuri,

Akitabasamu Yesu,

Kuna nuru moyoni.

Maandishi: Eliza E. Hewitt, 1851–1920

Muziki: John R. Sweney, 1837–1899

Isaya 60:19

Zaburi 16:9, 11

Chapisha