26
Enyi Wana wa Bwana
Kwa kushangilia
1. Enyi wana wa Bwana,
Tuimbe kwa umoja.
Tupaze wetu wimbo
Kwake atawalapo.
Tutasafishwa wote,
Na makosa yafutwe,
Tutapoacha dhambi,
Tuishi kwa amani.
2. Tutakavyofurahi
Tumwonapo Mwokozi!
Aja kwa utukufu,
Kukomesha maovu.
Nyimbo tutamwimbia
Mfalme wetu, Bwana.
Tutajaa upendo,
Woga kufika mwisho!
3. Tutakuwa wasafi,
Tutaishi nuruni.
Tutamwimbia sifa;
Shangwe tutazipaza.
Dunia isafishwe
Viumbe vyake vyote,
Viishi kwa upendo;
Furaha kila moyo.
Maandishi: James H. Wallis, 1861–1940
Muziki: Lahani ya Uhispania; umepangiliwa na Benjamin Carr, 1768–1831