49 Niongoze Kwa hamasa 1. Yesu, Mkombozi, Niongoze. Nakata shauri, Niongoze. Hata kwenye giza, Na kunapokucha. Uwe wangu mwanga. Niongoze. 2. Hata kwenye shida, Niongoze. Nifundishe wema. Niongoze. Nguvu ya wokovu Iwe kila siku, Bwana, kinga yangu. Niongoze. 3. Niwapo na dhambi, Niongoze. Nikiwa na jonzi, Niongoze. Inapotoweka Amani na raha, Nijaze neema, Niongoze. 4. Kikifika kifo, Niongoze. Nitulize moyo. Niongoze. Unihurumie Ili upendowe Kwako unilete. Niongoze. Maandishi na muziki: Orson Pratt Huish, 1851–1932 Alma 38:9 Zaburi 48:14