Muziki
Ukweli Ni Nini?


156

Ukweli Ni Nini?

Kwa ujasiri

1. Ukweli ni nini? Thamaniye

Huzidi vito na dhahabu,

Na ubora utaonekana pale

Ambapo utajiri wote wa falme

Utaonwa kama uchafu.

2. Ukweli ni nini? Tuzo zuri

Watu na mbingu kuwania.

Utafute ung’aripo kilindini,

Au ufukuzie hadi mbinguni:

Ni lengo la kutamaniwa.

3. Mwonevu nguvu atazidiwa

Ataposhindana na haki.

Hivyo ukweli utadumu daima,

Na ngome yake kuhimili vimbunga

Na mapinduzi ya katili.

4. Hivyo, ukweli ni mwisho na mwanzo,

Msimu, nyakati hauna.

Japo mbingu, nchi zitafika mwisho,

Ukweli, uhalisi, utakuwepo,

Kubakia hivyo, daima.

Maandishi: John Jaques, 1827–1900

Muziki: Ellen Knowles Melling, 1820–1905

Mafundisho na Maagano 93:23–28

Yohana 18:37–38

Chapisha