23 Sayuni Nzuri Mbinguni Kwa upole 1. Sayuni nzuri mbinguni; Napenda mji mzuri; Mizuri milango yake; Hekalu – Mungu nuruye; Aliyenipatanisha, Milango aifungua. [Chorus] A! Sayuni, ni kuzuri; Mji Sayuni; Sayuni, kwake Mungu! 2. Kuzuri mbinguni kote; Hata malaika wote; Nzuri nazo tumbuizo; Nzuri tarumbeta zao; Nitaimba na umati, Miguuni pa Mwokozi. [Chorus] A! Sayuni, ni kuzuri; Mji Sayuni; Sayuni, kwake Mungu! 3. Mazuri mataji yao, Matawi watandazayo; Wazuri wakombolewa, Wote wanaoingia; Nitaingia kwa hamu Kwenye pumziko langu. [Chorus] A! Sayuni, ni kuzuri; Mji Sayuni; Sayuni, kwake Mungu! Maandishi: George Gill, 1820–1880 Muziki: Joseph G. Fones, 1828–1906 Ufunuo 7:9–17 Ufunuo 21:2, 21–23