Muziki
Utukufu na Sifa


30

Utukufu na Sifa

Kwa ushindi

1. Utukufu na sifa

Mfalme ni vyako,

Wanao twakusifu

Hosana kwa Kristo.

Bwana wa Israeli,

Mwana wa Daudi,

Unayekuja Yesu,

Kama Mkombozi.

2. Kundi la malaika

Lakusifu juu,

Navyo viumbe vyote

Vyatoa majibu.

Kama Waebrania

Wabeba matawi,

Tunakupa upendo

Na sifa, Mwokozi.

3. Kabla ya kifo chako,

Waliimba sifa;

Sasa upo mbinguni,

Twakusifu Bwana.

Pokea sifa zetu,

Na pendo la kweli,

Kwako yote ni mema,

Mfalme mzuri.

Maandishi: Theodulph wa Orleans, 760–821

Muziki: Melchior Teschner, 1584–1635

Zaburi 148

Yohana 12:12–13

Chapisha