24 Katika Siku ya Shangwe Kwa furaha 1. Katika siku ya shangwe, Bwana, twakutukuza; Hapa ni patakatifu, Utukufu twaimba. [Chorus] Haleluya, Haleluya, Sauti tuzitoe, Tuimbeni kwa furaha Kwa Bwana na Mfalme! 2. Ifungue chemichemi; Zimwagike baraka, Kwa wakutumikiao Kwenye hii dunia. [Chorus] Haleluya, Haleluya, Sauti tuzitoe, Tuimbeni kwa furaha Kwa Bwana na Mfalme! 3. Tujenge ufalme wako, Alisema nabii, Kwamba wana wa ahadi Ndipo watapoishi. [Chorus] Haleluya, Haleluya, Sauti tuzitoe, Tuimbeni kwa furaha Kwa Bwana na Mfalme! Maandishi na Muziki: Leroy J. Robertson, 1896–1971. © 1980 IRI Zaburi 47:6–7 Alma 26:8, 16