18 Tumpendao Mungu Kwa furaha 1. Tumpendao Mungu, Njooni kwa furaha. Tumwimbie nyimbo tamu, Tumwabudu pamoja. 2. Kuna wale wageni Wasiojua neno. Sisi ndio watumishi Wakutangaza kwao. 3. Mungu ni Mtawala Wa dunia na mbingu, Kwa kauli hutuliza Dhoruba na ghadhabu. 4. Huyu Mwenyezi Bwana, Ndiye upendo wetu, Nguvu zake atatuma Kutupeleka juu. Maandishi: Isaac Watts, 1674–1748 Muziki: Aaron Williams, 1731–1776 Isaya 12:5 Warumi 8:28