12 Mungu Mbariki Kwa sala 1. Mungu mbariki Mpendwa nabii, Mpe afya. Na utuongoze sote Kwa maneno yake, Ili tuchague Yale mema. 2. Na wako ufalme, Uenee pote Ufikapo. Ukweli wawaka, Nasi twaungana, Kwa kasi kufika Kwenye lengo. 3. Tuwe na umoja, Kama Baba, Mwana, Kwa amani. Kwa mioyo yote, Tusimame sote, Na milele tuwe Majasiri. Maandishi: Bernard Snow, 1822–1894 Muziki: Harry A. Dean, 1892–1987.© 1985 IRI Mafundisho na Maagano 107:22 3 Nefi 19:23