139 Tusonge Mbele Kwa shauku 1. Tusonge mbele kwenye kazi ya Bwana, Ndipo tukaipate zawadi tukifa; Katika vita tuushike upanga, Upanga wa ukweli. [Chorus] Jipe moyo shinda adui Msihofu, Bwana yu nasi Hatutawasikiliza waovu Tutamtii Bwana Mungu. 2. Hatutasita ingawa tu wachache Tunapolinganishwa na adui kule; Katika Bwana nguvu yake tupate Kutetea ukweli. [Chorus] Jipe moyo shinda adui Msihofu, Bwana yu nasi Hatutawasikiliza waovu Tutamtii Bwana Mungu. 3. Hatutahofu tunapotenda mema, Kwa sababu Bwana yu karibu daima; Katika shida yeye atuwezesha Tuushike ukweli. [Chorus] Jipe moyo shinda adui Msihofu, Bwana yu nasi Hatutawasikiliza waovu Tutamtii Bwana Mungu. Maandishi na muziki: Evan Stephens, 1854–1930 Mafundisho na Maagano 6:33–37 1 Nefi 22:15–17