78 Kwa Upole Twaimba Kwa unyenyekevu 1. Kwa upole twaimba, Sabato yaja tena. Tupumzike, Tupumzike, Na tushukuru Mungu Baraka atupaye, Baraka atupaye. 2. Ndiyo siku teule, Mungu tumtafute, Ni thawabu, Ni thawabu, Na tule sakramenti Kumkumbuka Yesu, Kumkumbuka Yesu. 3. Tuongeze sauti Tuletapo zawadi Ya upole, Ya upole, Kama dhabihu yetu Ni kwa neema yake, Ni kwa neema yake. 4. Ni mtukufu Kristo; Ni zuri lake neno: Fanya toba, Fanya toba; Japo dhambi nyekundu, Msamaha atoa. Msamaha atoa. Maandishi: William W. Phelps, 1792–1872. Yalijumuishwa katika kitabu cha kwanza cha nyimbo za Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, 1835. Muziki: Thomas C. Griggs, 1845–1903 Mafundisho na Maagano 59:8–12 Isaya 1:16–18