Muziki
Bwana, Dhoruba Yavuma


53

Bwana, Dhoruba Yavuma

Kwa hamasa

1. Bwana, dhoruba yavuma!

Mawimbi ni makali!

Na giza limetanda mbingu.

Hifadhi ipo mbali.

Hujali twaangamia?

Walalaje foo,

Hali kila dakika yatisha

Na tishio la kifo?

[Chorus]

Upepo, mawimbi yaitika:

Nyamaza.

Ghadhabu ya tufani, iwe

Pepo chafu, watu au chochote,

Hakuna maji ya kumdhuru

Bwana wa bahari, nchi, mbingu.

Vyote vitakuitikia:

Nyamaza, tulia.

Vyote vitakuitikia:

Tulizana.

2. Bwana, kwa majonzi mengi

Leo nanyenyekea.

Moyo umejaa taabu.

Niokoe, naomba!

Mabubujiko ya dhambi

Yalemea roho,

Nafa maji! Nazama! Ee Bwana.

Ninyoshee mkono!

[Chorus]

Upepo, mawimbi yaitika:

Nyamaza.

Ghadhabu ya tufani, iwe

Pepo chafu, watu au chochote,

Hakuna maji ya kumdhuru

Bwana wa bahari, nchi, mbingu.

Vyote vitakuitikia:

Nyamaza, tulia.

Vyote vitakuitikia:

Tulizana.

3. Bwana, vitisho vyakoma.

Hali sasa tulivu.

Jua la akisi ziwani,

Moyoni sina hofu.

Kawia, Bwana mpendwa!

Nitoe upweke,

Nifikie bandari ya kheri

Pwani nipumzike.

[Chorus]

Upepo, mawimbi yaitika:

Nyamaza.

Ghadhabu ya tufani, iwe

Pepo chafu, watu au chochote,

Hakuna maji ya kumdhuru

Bwana wa bahari, nchi, mbingu.

Vyote vitakuitikia:

Nyamaza, tulia.

Vyote vitakuitikia:

Tulizana.

Maandishi: Mary Ann Baker, 1831–1921

Muziki: H. R. Palmer, 1834–1907

Mathayo 8:23–27

Marko 4:36–41

Chapisha