7 Israeli, Mnaitwa Kwa ari 1. Israeli, mnaitwa Na Mwenyezi mtubu. Babiloni yaanguka; Inakuja hukumu. Njooni humu Sayuni, Kabla yake gadhabu. Njooni humu Sayuni, Kabla yake gadhabu. 2. Israeli, sikiliza Bwana asema nawe! Asubuhi yaangaza Kwa Wateule wote. Njooni humu Sayuni, Ndani mfurahie. Njooni humu Sayuni, Ndani mfurahie. 3. Israeli, malaika Toka juu washuka, Wakiwapa Wema nguvu Ya kurudi kwa Baba. Njooni humu Sayuni, Bwana wenu yu aja. Njooni humu Sayuni, Bwana wenu yu aja. 4. Israeli, msibaki Katika dhambi zenu! Ona! Hukumu ya haki Yaja hivi karibu. Njooni humu Sayuni! Bwana Mungu msifu. Njooni humu Sayuni! Bwana Mungu msifu. Maandishi: Richard Smyth, 1838–1914 Muziki: Charles C. Converse, 1832–1918 Mafundisho na Maagano 133:7–16