162 Mahekalu ya Sayuni Kwa ujasiri 1. Mahekalu ya Sayuni Yang’ara utukufu, Njia ya kwenda mbinguni, Alama ya uungu. Taswira ya kuvutia Yatuita kuomba; Watiifu wa ahadi, Pale tutatumika. 2. Mungu Baba wa rehema, Tutakase twaomba; Bariki dhamira yetu Ya ndugu kuokoa, Hadi siku watiifu, Wote tuliofungwa Kwa pingu za selestia, Tuziimbe hosana. 3. Mbingu, imba kwa sauti, Nyimbo za kumsifu Mfalme Imanueli! Imba Watakatifu! Milima ishangilie Na konde zifurahi, Nyota nazo zimsifu Ameshinda kaburi. Maandishi: Archibald F. Bennett, 1896–1965. © 1948 IRI Muziki: Alexander Schreiner, 1901–1987. © 1948 IRI Mafundisho na Maagano 138:47–48 Mafundisho na Maagano 128:22–24