106
Nastaajabu
Kwa kutafakari
1. Nastaajabu upendo wa Yesu kwangu,
Nashangaa neema yake timilifu.
Yasisimua kwamba alisulubiwa,
Kwa ajili yangu, aliteswa na kufa.
[Chorus]
Ni ajabu kwangu angenithamini
Kiasi cha kufa!
Ni ajabu kwangu, ajabu sana!
2. Nastaajabu kwamba angetoka juu
Kuokoa nafsi kiburi kama yangu,
Kwamba upendo wake angenionesha,
Kunikomboa, hata kunihalalisha.
[Chorus]
Ni ajabu kwangu angenithamini
Kiasi cha kufa!
Ni ajabu kwangu, ajabu sana!
3. Nawaza mikono yake ilivyochomwa!
Nisahauje upendowe na huruma?
Hata! Nitamtukuza na kumsifu,
Hadi miguuni nitapomsujudu.
[Chorus]
Ni ajabu kwangu angenithamini
Kiasi cha kufa!
Ni ajabu kwangu, ajabu sana!
Maandishi na muziki: Charles H. Gabriel, 1856–1932
Yohana 15:13