20 Njooni Enyi Watakatifu Kwa ujasiri 1. Njooni enyi Watakatifu; Kwa moyo tembea. Safari yaweza kuwa ngumu, Neema yatosha. Ni bora tuvumilie Wasiwasi tuondoe; Fanya hivi, mfurahi— Ni shwari! Ni shwari! 2. Je, tulijutie fungu letu? Si hivyo; ni sawa. Je, tuitegemee thawabu, Vitani twatega? Dhamiria; jipe moyo. Mungu wetu nasi yupo; Punde itanenwa hivi— Ni shwari! Ni shwari! 3. Tutayapata makao mapya, Sayuni tufike, Ambapo hatutasumbuliwa; Baraka tupate. Tutapaza nyimbo zetu Kumsifu Mungu wetu; Na tutasema zaidi— Ni shwari! Ni shwari! 4. Na tukifa kabla ya kufika, Hakika! Ni shwari! Tutakuwa huru, bila shida, Tuishi peponi! Na kama tutakuwepo Kuliona kimbilio Tutaimba jinsi gani— Ni shwari! Ni shwari! Maandishi: William Clayton, 1814–1879 Muziki: Wimbo wenye asili ya Uingereza Mafundisho na Maagano 61:36–39 Mafundisho na Maagano 59:1–4