16 Msikilize Nabii Kwa furaha 1. Msikilize nabii Na neno la Mungu, Ufurahie ukweli Uimbe kwa nguvu. Tumeshaipata njia Ya wale wa mwanzo. Nabii mpya katumwa Kurejesha neno. 2. Giza nene lilitanda Kote duniani, Bwana amelifukuza, Mungu anaishi. Kupitia njama mbovu Zikawapotosha, Lakini Watakatifu Wamepata njia. 3. Hawategemei mtu Na yake mikono. Wamkataao Yesu, Laana ni yao. Anasema Mkombozi, “Nifuate, njoo, Neno langu ulitii Hata mpaka mwisho”. 4. Sikia neno la kweli Safi vyanzo vyake. Amri zake uzitii Hadi uteule, Na uvalishwe na Mungu Taji la milele, Utapata utukufu, Urithi wa shangwe. Maandishi: Joseph S. Murdock, 1822–1899. Ubeti wa nne, Bruce R. McConkie, 1915–1985. © 1985 IRI Muziki: Joseph J. Daynes, 1851–1920 Joseph Smith—Historia ya 1:14–17 Mafundisho na Maagano 21:4–7