Mafundisho na Maagano 2021
Aprili 12–18. Mafundisho na Maagano 37–40: “Kama Hamna Umoja Ninyi Siyo Wangu”


“Aprili 12–18. Mafundisho na Maagano 37–40: ‘Kama Hamna Umoja Ninyi Siyo Wangu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Aprili 12–18. Mafundisho na Maagano 37–40,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2021

Picha
Watakatifu wakijiandaa kuhama

Watakatifu Wanahamia Kirtland, na Sam Lawlor

Aprili 12–18

Mafundisho na Maagano 37–40

“Kama Hamna Umoja Ninyi Siyo Wangu”

Kabla ya kupanga kile utakachofanya darasani, jifunze kwa maombi Mafundisho na Maagano 37–40. Kuna uwezekano mkubwa wa kupokea mwongozo wa kiroho katika kujiandaa kwako kufundisha kama utaanza kwa kuwa na uzoefu wa maana na maandiko haya.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Fikiria kuandika ubaoni, Nilipokuwa nikisoma Mafundisho na Maagano 37–40, Nilihisi kwamba Bwana alikuwa ananiambia . Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki jinsi wangekamilisha sentensi hiyo. Wahimize kushiriki mstari kutoka kujifunza kwao kama sehemu ya majibu yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 37–38

Mungu hutukusanya ili atubariki.

  • Wakati mwingine ni rahisi kujifunza kutoka kwenye ufunuo katika Mafundisho na Maagano wakati tunapojiona katika nafasi za watu ambao kiasili ulitolewa kwao. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kufanya hivi pamoja na sehemu za 37–38, ungeweza kuwaalika wafikirie kwamba wanaishi kule Fayette, New York, mnamo mwaka wa 1831. Mshiriki wa darasa angeweza kujifanya kuwa Joseph Smith na awasomee sehemu ya 37. Ni kwa jinsi gani tungejibu amri hii? Labda washiriki wa darasa wangeweza kujifanya kwamba wanaye rafiki ambaye hataki kukusanyika Ohio; wangeweza kupekua sehemu ya 38 kwa ajili ya kanuni ambazo zinaweza kumhimiza rafiki yao kuwa mwaminifu katika amri ya kukusanyika. (Ikihitajika, ungeweza kuwaelekeza hasa kwenye mistari ya 1–4, 11–12, 17–22, na 27–33.) Washiriki wa darasa pia wanaweza kuwa tayari kushiriki jinsi kanuni sawa na hizo zimewasaidia wakati walihitaji kutii amri ambayo ilionekana kuwa ngumu.

  • Watakatifu wa Siku za Mwisho hawaamriwi tena kukusanyika kwa kuhamia eneo moja, lakini tungali tunakusanyika katika familia, kata, na vigingi. Kujadili jinsi kukusanyika huku kunatubariki leo hii, ungeweza kuligawa darasa katika makundi mawili. Liombe kundi moja lipekue Mafundisho na Maagano 38:31–33 na kutafuta baraka ambazo zinazohusiana na kukusanyika kama familia, na uliombe lile kundi jingine kupekua kifungu hicho pia na watafute baraka zinazohusiana na kukusanyika kama kata na vigingi. Kisha wangeweza kushiriki mawazo yao na darasa. Ni kwa jinsi gani tunabarikiwa kwa kukusanyika pamoja kama darasa la Shule ya Jumapili?

Mafundisho na Maagano 38:24–27

Watu wa Mungu lazima wawe kitu kimoja.

  • Watakatifu ambao walikusanyika kule Ohio walikuja kutoka katika hali tofauti, lakini Mungu aliwaamuru kuweka kando tofauti zao na “wawe na umoja” (mstari wa 27). Kwa nini wakati mwingine tunakosa kuona watu wengine wakiwa sawa na sisi? Wahimize washiriki wa darasa kutafakari jinsi wanavyowatendea wengine wanaposoma Mafundisho na Maagano 38:24–27. Je, inamaanisha nini kuwapenda kaka zetu na dada zetu kama vile tunavyojipenda. Kwa nini haiwezekani kiukweli kuwa watu wa Mungu kama hatuna umoja?

  • Kusoma Mafundisho na Maagano 38:24–27 kunaweza elekeza kwenye mjadala kuhusu umoja katika mahusiano yetu—kama washiriki wa kata, familia, na kadhalika. Video “A Friend to All” au “Love in Our Hearts” kwenye ChurchofJesusChrist.org zaweza zikasaidia. Kwa mfano, washiriki wa darasa wangeweza kushiriki kauli au misukumo kutoka kwenye video ambayo inawasaidia kuelewa vyema zaidi kanuni katika mistari ya 24–27. Pia wangeweza kutafakari na kushiriki mawazo kuhusu swali kama “Naweza kufanya nini kuisaidia kata yetu kuhisi umoja zaidi.

Mafundisho na Maagano 38:39; 39–40

Baba wa Mbinguni anataka kutupatia utajiri wa milele.

  • Kutengeneza jedwali kunaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kujadili Mafundisho na Maagano 38:39. Katika safu moja, washiriki wa darasa wangeweza kuorodhesha “utajiri wa ulimwengu,” au vitu ambavyo vinatambulika kuwa vya thamani duniani lakini havidumu kufikia maisha yajayo. Katika hiyo safu nyingine, wangeweza kuorodhesha “utajiri wa milele,” au vitu ambavyo Mungu anavithamini na ambavyo vinaweza kudumu milele. Ni uzoefu gani umetufundisha kwamba utajiri wa milele ni wa thamani kuliko utajiri wa ulimwengu?

  • James Covel, kama wengi wetu, alikuwa na matamanio ya haki. Lakini kukosa kwake kutii agizo la Mungu ni onyo muhimu kwetu sisi wote. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kujifunza kutoka kwenye uzoefu wa Covel, ungeweza kuwaalika baadhi yao wapekue sehemu ya 39 kwa ajili ya vitu ambavyo Bwana alimtaka avifanye. Wengine wangeweza kuchunguza baraka alizoahidiwa kama angetii. Pia wangeweza kupekua sehemu ya 40 kugundua kwa nini James Covel hakupokea baraka hizi. Ni kwa jinsi gani uzoefu wake unaweza kutumika kwetu? Ni “shughuli [gani] za ulimwengu” wakati mwingine hutuzuia kupokea neno la Mungu “kwa furaha”? (Mafundisho na Maagano 40:2).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Usijaribu kufundisha kila kitu. “Kuna mengi ya kujadili katika kila somo, lakini siyo lazima kushughulikia kila kitu katika wakati mmoja darasani ili kugusa moyo wa mtu—mara nyingi kipengele kimoja au viwili muhimu huwa vinatosha” (Kufundisha Katika Njia ya Mwokozi, 7). Roho Mtakatifu, maoni kutoka kwa washiriki wa darasa, na mawazo katika mwongozo huu vinaweza kukusaidia kujua wapi ufokasi.

Chapisha