Mafundisho na Maagano 2021
Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66: “Bwana Anahitaji Moyo na Akili Yenye Kukubali”


“Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66: ‘Bwana Anahitaji Moyo na Akili Yenye Kukubali,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Juni 14–20. Mafundisho na Maagano 64–66,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2021

Picha
shamba wakati wa machweo

Wilaya ya Daviess, Missouri

Juni 14–20

Mafundisho na Maagano 64–66

“Bwana Anahitaji Moyo na Akili Yenye Kukubali”

Utakapokuwa ukijifunza wiki hii, kwa sala zingatia kanuni zipi kutoka Mafundisho na Maagano 64–66 zinaweza kuongeza imani na ufahamu wa washiriki wa darasa lako.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Ili kuwahimiza washiriki wa darasa kushiriki kitu walichokipata kuwa cha maana wakati wakijifunza maandiko wiki hii, unaweza kuwauliza changamoto tunazokabiliana nazo leo. Kisha waalike kushiriki mstari kutoka Mafundisho na Maagano 64–66 ambao wanahisi unaweza kuwa msaada kwa mojawapo ya changamoto hizo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 64:1–11

Tunahitajika kusamehe watu wote.

  • Labda washiriki wa darasa wanaweza kufaidika kutokana na kuzungumza kuhusu kwa nini kuwasamehe wengine kunaweza kuwa vigumu sana—na jinsi ambavyo wameshinda changamoto hizo. Wanaweza kuchunguza Mafundisho na Maagano 64:1–11 kwa ajili ya kanuni na kweli ambazo zinawatia msukumo wao kuwa wenye kusamehe zaidi. Je, tunajifunza nini kuhusu Mwokozi kutoka kwenye mistari hii? Ili kusaidia kuonesha baraka za msamaha, unaweza kushiriki hadithi ya Morrell Bowen kutoka kwenye ujumbe wa Mzee Jeffrey R. Holland “Huduma ya Upatanisho” (Ensign au Liahona, Nov. 2018, 77–79) au video “Forgiveness: My Burden Was Made Light” (ChurchofJesusChrist.org). Au mshiriki wa darasa anaweza kuwa tayari kushiriki hadithi binafsi ya kutoa au kupokea msamaha. Ni kwa jinsi gani watu katika mifano hii walibarikiwa kwa uwezo wa kutoa msamaha?

Mafundisho na Maagano 64:31–34

Bwana anahitaji kutoka kwetu “moyo na akili yenye kukubali.”

  • Bwana hataki “tuchoke”; hata hivyo, ni kawaida kwa watu ambao wanajaribu kadri ya uwezo wao—ikijumuisha, labda, baadhi katika darasa lako—kuwa wenye “kuchoka kutenda mema.” Kwa nini kuchoka kunatokea? Tunapata ushauri gani katika Mafundisho na Maagano 64:31–34 ambao unaweza kutusaidia tunapopambana na hisia kama hizi?

  • Ili kuboresha mjadala wenu, unaweza kuonesha picha za kitu kikubwa na cha kupendeza ambacho kilijengwa kwa muda mrefu kwa kutumia “vitu vidogo”—kama vile nakshi au nyumba ya matofali. Ni nini baadhi ya mifano ya “kazi kubwa” ambayo Bwana ametupatia? Ni vitu gani vidogo tunaweza kufanya ili kujenga msingi wa kazi hiyo?

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kutafakari kwa kina zaidi kuhusu Mafundisho na Maagano 64:34, unaweza kuandika Moyo na Akili Yenye Kukubali kwenye ubao. Washiriki wa darasa wanaweza kuorodhesha chini ya vichwa hivi vya habari kile wanachohisi inamaanisha kutoa mioyo na akili zetu zenye kukubali kwa Bwana. Kwa ajili ya maelezo ya istilahi hizi, ona maneno ya Mzee Donald L. Hallstrom katika “Nyenzo za Ziada.” Maandiko kama yafuatayo yanaweza kutupatia umaizi: Mosia 7:33; Etheri 4:15; Mafundisho na Maagano 43:34; Musa 7:18; Historia ya—Joseph Smith1:19.

Mafundisho na Maagano 65

Ufalme wa Mungu duniani hutayarisha ulimwengu kwa ajili ya kurudi kwa Mwokozi.

  • Mafundisho na Maagano 65 inatoa ufafanuzi wa kutia msukumo wa misheni ya Kanisa la Bwana katika Siku za Mwisho. Kuwasaida washiriki wa darasa kuona sehemu yao katika misheni hii, unaweza kuwaalika wachunguze sehemu ya 65 wakitafuta majibu kwa maswali kama haya: Ni nini Bwana anataka Ufalme Wake utimize duniani? Ni nini anataka nifanye ili kutoa msaada? Mnaweza kutazama video “Prepare Today for the Second Coming” (ChurchofJesusChrist.org) au mrejelee ujumbe wa Rais Dallin H. Oaks katika “Nyenzo za Ziada.” Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki jinsi ambavyo wangejibu maswali ya Rais Oaks.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

“Moyo na akili yenye kukubali.”

Mzee Donald L. Hallstrom alipendekeza maana hii ya karibu ya kirai “moyo na akili yenye kukubali”:

“Moyo huashiria upendo na kujitolea. Tunatoa dhabihu na kubeba mizigo ya wale tunaowapenda ambayo tusingeivumilia kwa sababu nyingine yeyote. Kama hakuna upendo, kujitolea kwetu hufifia. …

“Kuwa na ‘akili yenye kukubali’ ina maana kujitolea kwa uwezo wetu wote na fikra zetu bora na kutafuta busara ya Mungu. Inapendekeza kuwa kujifunza kwetu kwa bidii katika maisha yetu yote kunapaswa kuwa juu ya vitu ambavyo ni vya milele kiasili. Inamaanisha kwamba ni lazima kuwe na uhusiano usiochanganulika baina ya kulisikia neno la Mungu na kulitii” (“Moyo na Akili Yenye Kukubali,” Ensign, Juni 2011, 31–32).

Matayarisho kwa ajili ya Ujio wa Pili.

“Vipi kama siku ya kuja Kwa [Yesu Kristo] ingekuwa kesho? Kama tungejua kwamba tungekutana na Bwana kesho—kupitia kifo chetu katika umri mdogo au kupitia ujio Wake usiotarajiwa —je tungefanya nini leo? Je, tungeungama juu ya nini? Ni mazoea gani ambayo tungesitisha? Ni madeni yapi ambayo tungekamilisha? Ni misamaha ipi ambayo tungetoa? Ni shuhuda zipi ambazo tungetoa?” (Dallin H. Oaks, “Preparation for the Second Coming,” Ensign au Liahona, Mei 2004, 9).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Kuvuta nguvu kutoka kwa Kristo. Katika juhudi zako za kuishi na kufundisha zaidi kama Mwokozi, wakati mwingine ni vigumu kuepuka kukosea. Usikate tamaa; bali, acha makosa na mapungufu yako yakuelekeze kwa Baba wa Mbinguni na Mwokozi” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,14).

Chapisha