Mafundisho na Maagano 2021
Juni 21–27. Mafundisho na Maagano 67–70: “Thamani … Utajiri wa Ulimwengu Wote”


“Juni 21–27. Mafundisho na Maagano 67–70: ‘Thamani … Utajiri wa Ulimwengu Wote,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Juni 21–27. Mafundisho na Maagano 67–70,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili

Picha
revelation manuscript book in display case

Juni 21–27

Mafundisho na Maagano 67–70

“Thamani … Utajiri wa Ulimwengu Wote”

Kujitayarisha kufundisha inamaanisha zaidi ya kufikiria kuhusu kile utakachosema na kutenda kama mwalimu. Kunapaswa pia kujumuisha kufikiria kile wanafunzi wanachoweza kufanya ili kufundishana wao kwa wao. Ni jinsi gani utawaalika washiriki wa darasa kushiriki uzoefu au umaizi ambao waliupata waliposoma maandiko haya?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Unaweza kuandika kwenye ubao Wiki hii Bwana alinifundisha … na uwaalike washiriki wa darasa wakamilishe sentensi kwa kitu walichojifunza.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 67:1–9

Funuo zilizotolewa kupitia Joseph Smith ni za kweli na zinatoka kwa Mungu.

  • Kuelewa historia ya Mafundisho na Maagano 67 kunaweza kuwa msaada kwenye mjadala kuhusu sehemu hii. Pengine mshiriki wa darasa anaweza kufupisha hali ambazo zilichangia ufunuo huu (ona Mafundisho na Maagano 67, kichwa cha habari cha sehemu; Watakatifu, 1:140–43). Kama tungekuwa katika mkutano ambapo kuchapishwa kwa ufunuo kulijadiliwa, ni sababu zipi tungetoa kuunga mkono wazo hilo? Tunaweza kuwaambia nini watu ambao wana shaka kuhusu dosari katika lugha ya Joseph Smith? Ni nini sehemu ya 67 inafundisha kuhusu manabii na ufunuo? Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki namna walivyokuja kujua wao wenyewe kuwa funuo hizi ni za kweli.

Mafundisho na Maagano 68:1–6

Maneno yenye msukumo ya watumishi wa Bwana ni maneno ya Bwana.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kujadili Mafundisho na Maagano 68:1–6, unaweza kuwaalika wasome mistari hii katika vikundi vidogo na washiriki wao kwa wao kweli wanazojifunza kuhusu mafundisho ya watumishi wa Bwana. Alika vikundi kushiriki wao kwa wao jinsi walivyojua kanuni zinazofundishwa katika mstari wa 4 ni za kweli. Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki uzoefu wa wakati ambapo walizungumza au kufundisha kama “walivyoongozwa na Roho Mtakatifu” (mstari wa 3) na jinsi Mungu alivyokuwa nao na kusimama karibu nao (ona mstari wa 6).

  • Kama ungependa kujadili namna ambavyo mistari hii inatumika kwenye mafundisho ya watumishi wa Bwana katika mkutano mkuu, kauli ya Mzee Jeffrey R. Holland katika “Nyenzo za Ziada” inaweza kuwa yenye kusaidia. Washiriki wa darasa pia wangeweza kushiriki ujumbe wa hivi karibuni kutoka kwenye mkutano ambao uliimarisha imani yao kwenye mafundisho yanayopatikana katika mistari hii.

Mafundisho na Maagano 68:25–31

Wazazi wana jukumu la kuwafunza watoto wao.

  • Je, kuna wazazi katika darasa lako—au wazazi watarajiwa? Labda ungeweza kufaidika kutokana na kuzungumza kuhusu ushauri wa Bwana kwa wazazi katika sehemu ya 68. Kwa mfano, labda baadhi ya wazazi katika darasa wangechagua kanuni kutoka mistari 25–28 na kuzungumza kuhusu jinsi ambavyo wao hujaribu kufundisha vitu hivi kwa watoto wao (mistari 29–31 pia ina baadhi ya kanuni muhimu). Au washiriki wa darasa wanaweza kuzungumza kuhusu jinsi ambavyo wazazi wao wamewafundisha kanuni za injili.

    Kwa nini nyumbani ni sehemu bora zaidi kwa ajili ya watoto kujifunza injili? Ni nini tunaweza kusema kwa wazazi ambao wanahisi wenye mapungufu au kuzidiwa na jukumu la kuwafundisha watoto wao?

    Picha
    familia ikijifunza

    Mungu amewapa wazazi jukumu la kufundisha watoto wao.

Mafundisho na Maagano 70:1–4

Tunawajibika kwa ajili ya funuo ambazo Bwana ametupatia?

  • Bwana aliwapatia ndugu fulani usimamizi juu ya funuo hizo kuzipeleka kule Missouri na kusimamia uchapishaji wake. Ni kwa namna gani tunaweza kujiona sisi wenyewe kama walinzi wa funuo hizo? Ni mafunzo gani mengine kuhusu utumishi kutoka sehemu hii yanatufaa sisi?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Mungu huzungumza nasi leo.

Mzee Jeffrey R. Holland alishiriki jinsi kanuni inayofundishwa katika Mafundisho na Maagano 68:4 inavyotumika kwenye mkutano mkuu: “Ninawaomba mtafakari katika siku zijazo si tu juu ya jumbe ambazo mmesikia lakini pia juu ya tukio la kipekee ambalo ndilo mkutano mkuu—kile ambacho sisi kama Watakatifu wa Siku za Mwisho tunaamini mikutano kama hiyo kuwa na kile tunachoalika dunia kukisikia na kukitazama. Tunatoa ushuhuda kwa kila taifa, kabila, lugha, na watu kwamba Mungu si tu anaishi lakini pia Anazungumza, kwamba kwa wakati wetu na katika siku yetu ushauri ambao umeusikia leo uko, chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu, ‘mapenzi ya Bwana, … neno la Bwana, … sauti ya Bwana, na uweza wa Mungu kwa wokovu’ [Mafundisho na Maagano 68:4]” (“Bendera kwa Mataifa,” Ensign au Liahona, Mei 2011, 111).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie wanafunzi ili wainuane. “Kila mtu katika darasa lako ni chanzo kikubwa cha ushuhuda, umaizi, na uzoefu kutokana na kuishi injili. Waalike kushiriki wao kwa wao na kuinuana” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,5).

Chapisha