Mafundisho na Maagano 2021
Julai 5–11. Mafundisho na Maagano 76: “Tuzo Lao Litakuwa Kuu na Utukufu Wao Utakuwa wa Milele”


“Julai 5–11. Mafundisho na Maagano 76: ‘Tuzo Lao Litakuwa Kuu na Utukufu Wao Utakuwa wa Milele,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Julai 5–11. Mafundisho na Maagano 76,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2021

Picha
kundi la nyota angani

Kimbilio, na Shaelynn Abel

Julai 5–11

Mafundisho na Maagano 76

“Tuzo Lao Litakuwa Kuu na Utukufu Wao Utakuwa wa Milele”

Sawa na maono mengi yaliyorekodiwa katika maandiko, ono katika sehemu ya 76 lilitokea wakati Joseph Smith na Sidney Rigdon “wakitafakari” maandiko (mstari wa 19). Wewe pia unaweza kupokea ufunuo—ikiwa ni pamoja na mwongozo kuhusu namna ya kufundisha—unapotafakari Mafundisho na Maagano 76.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuzungumza kuhusu kile walichosoma katika Mafundisho na Maagano 76, ungeweza kuwaalika kufikiria kwamba rafiki wa imani tofauti anauliza kile tunachoamini kuhusu maisha baada ya kifo. Ni mistari gani kutoka sehemu ya 76 wangeshiriki na rafiki yao? Washiriki wa darasa wanaweza pia kushiriki kitu kutoka “Sauti za Urejesho: Shuhuda za ‘Ono’” ambacho kiliwavutia.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 76

Wokovu huja kupitia Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

  • Watu wengi, wakati wanapofikiri kuhusu sehemu ya 76, wanafikiri kuhusu mpango wa wokovu na falme tatu za utukufu. Unawezaje kuwasaidia washiriki wa darasa kuona kwamba mtu mkuu katika ufunuo huu ni Mwokozi Yesu Kristo? Ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki mstari walioupata katika sehemu ya 76 ambao uliimarisha imani yao katika Yesu Kristo. Kama wanahitaji msaada, ungeweza kuwaelekeza kwenye mistari kama 1–5, 20–24, 39–43, 69, 107–8.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuchunguza tofauti baina ya wale wanaorithi falme hizo tatu za utukufu, andika kwenye ubao Selestia, mistari 50–70, 92–96; Terestria, mistari 71–79, 97; na Telestia, mistari 81–90, 98–106, 109–12. Washiriki wa darasa wanaweza kuchagua mojawapo ya seti hizi za mistari na kutafuta virai ambavyo vinaelezea uhusiano baina ya Yesu Kristo na watu wanaorithi ufalme unaohusika. Je, virai hivi vinatufundisha nini kuhusu kuwa wafuasi wa Yesu Kristo? Tunawezaje kuimarisha uhusiano wetu na Yeye pamoja na Baba? Ni kwa jinsi gani Wanatusaidia? Inamaanisha nini kuwa “jasiri katika ushuhuda wa Yesu”? (mstari wa 79).

    Picha
    chumba katika nyumba ya karne ya kumi na tisa

    Joseph Smith alipata ono la falme za utukufu ndani ya chumba kama hiki.

Mafundisho na Maagano 76:5–10, 113–18

Siri za Mungu zinaweza tu “kueleweka kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.”

  • Yaweza kuwa ya kupendeza washiriki wa darasa lako kujua kwamba si waumini wote wa Kanisa walikubali kwa urahisi ufunuo katika sehemu ya 76. Kwa mfano, Brigham Young alisema: “Desturi zangu zilikuwa hivi, kwamba wakati Ono lilipokuja kwanza kwangu, lilikuwa moja kwa moja kinyume na lilipingana na elimu yangu ya awali. Nilisema, Subiri kidogo. Sikulikataa; lakini sikulielewa.” Alisema kwamba alihitaji “kufikiri na kusali, kusoma na kufikiri, hadi alipojua na kuelewa yeye mwenyewe” (katika “Ono,” Ufunuo katika Muktadha, 150). Tunajifunza nini kutoka kwenye uzoefu wake kinachoweza kutusaidia wakati Mungu anapofunua vitu ambavyo ni tofauti na uelewa wetu wa sasa? Ni nini Mafundisho na Maagano 76:5–10, 113–18 inatufundisha kuhusu jinsi tunavyoweza kupokea “siri za mapenzi ya [Mungu]”? (mstari wa 10).

Mafundisho na Maagano 76:50–70; 92–95

Mungu anataka watoto Wake wote wafurahie utukufu wa selestia pamoja Naye.

  • Kwa baadhi, inaweza kuvunja moyo au kugharikisha kufikiria kuhusu kila kitu kinachohitajika kwetu ili tuwe wastahiki wa ufalme wa selestia. Fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia washiriki wa darasa kutafuta amani “kwa njia ya Yesu aliye mpatanishi” (mstari wa 69). Kwa mfano, unaweza kuwaalika wasome mistari 50–70 na 92–95. Waalike kushiriki jinsi ambavyo wanaweza kumjibu mtu anayesema, “Kuishi injili katika dunia ya sasa ni vigumu sana; Sina uhakika kama ina thamani” au “Mimi sistahili ufalme wa selestia.” Tunaweza kusema nini ili kumtia msukumo au kumtia moyo mtu huyu?

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fokasi kwa Mwokozi na Mafundisho Yake. “Kila mara jiulize, ‘Ni kwa jinsi gani kile ninachofundisha kitawasaidia washiriki wa darasa langu kujenga imani katika Kristo, kutubu, kufanya na kushika maagano na Mungu, na kupokea Roho Mtakatifu?’” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 20).

Chapisha