Agano la Kale 2022
Aprili 4–10. Kutoka 14–17: “Simameni Kimya, na Muone Wokovu wa Bwana”


“Aprili 4–10. Kutoka 14–17: ‘Simameni Kimya, na Muone Wokovu wa Bwana,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Aprili 4–10. Kutoka 14–17,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
Bahari ya Shamu

Bahari ya Shamu

Aprili 4–10

Kutoka 14–17

“Simameni Kimya, na Muone Wokovu wa Bwana”

Fikiria kuhusu jinsi uzoefu wa wana wa Israeli unavyotumika kwa washiriki wa darasa lako. Ni uzoefu gani utakuwa wa msaada mno kwao kujadili?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kutoka 14–17 imejazwa na maelezo ya kukumbukwa. Mshiriki wa darasa angeweza kuchora picha ya tukio kutoka sura hizi wakati washiriki wengine wa darasa wakikisia nini yeye anachokichora. Waombe kushiriki kile walichojifunza kutokana na maelezo hayo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Kutoka 14

Baba wa Mbinguni hutuokoa tunapomfuata Roho.

  • Bahari ya Shamu ilionekana kama mwisho wa Waisraeli, lakini Mungu alijua vitu wasivyovijua. Kurejea upya maelezo ya uvukaji wa kimiujiza wa Bahari ya Shamu kungeweza kuwakumbusha washiriki wa darasa juu ya nyakati Mungu alipowakomboa kutokana na majaribu yao. Ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kurejea upya Kutoka 14 na kushiriki kile kinachowavutia zaidi kuhusu maelezo haya. Pia watie moyo kushiriki uzoefu wao wa kukombolewa kutoka kwenye majaribu, pamoja na mistari kutoka kwenye sura ambayo inajenga imani yao kwamba Mungu anaweza kutukomboa sisi.

  • Inaweza pia kuvutia kusoma pamoja Mafundisho na Maagano 8:2–3. Mistari hii inafundisha nini kuhusu Musa? Jinsi gani mistari hii inaathiri tunavofikiri kuhusu matukio katika Kutoka 14? Inapendekeza nini kuhusu jinsi tunavyotafuta ukombozi kutokana na majaribu yetu? Fikiria kile ambacho maelezo katika “Nyenzo za Ziada” yangeweza kuongezea kwenye mjadala wenu.

Picha
Mwanamke akikusanya mana

Mana kutoka kwa Mungu iliwashibisha Waisraeli kimwili; sisi pia tunahitaji chakula cha kiroho kila siku. Fresco na Leopold Bruckner

Kutoka 15:23–27; 16:1–15; 17:1–7

Bwana atakidhi mahitaji yetu tunaposafiri kupitia maisha.

  • Kutoka 15–17 inatupa maelezo mengi ambayo yanaweza kujenga imani ya washiriki wa darasa katika uwezo wa Bwana na utayari wake kukidhi mahitaji yetu ya kimwili na kiroho. Pengine kila mshiriki wa darasa angeweza kujifunza moja ya vifungu vifuatavyo, akitafuta jumbe za kiroho: Kutoka 15:23–27; 16:1–15; 17:1–7. Wape baadhi ya washiriki wa darasa nafasi ya kushiriki kile walichopata. Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kutumia maelezo haya kumtia moyo mtu fulani ambaye ana mahitaji yake ya kimwili au kiroho ambayo hayajatimizwa?

  • Washiriki wa darasa wangeweza pia kusoma mistari hii na kutambua mifano ya kunu’gunika. Jinsi gani tunaweza kuelezea kwa mtu fulani ina maanisha nini kunu’gunika? Nini baadhi ya matokeo ya kunun’gunika ambayo yanaleta hatari kubwa? Pengine washiriki wa darasa wangeweza kushiriki ushauri juu ya jinsi ya kuepuka jaribu la kunun’gunika dhidi ya Bwana tunapokabiliana na majaribu magumu.

  • Inaweza kusaidia washiriki wa darasa kufananisha mana iliyoelezwa katika Kutoka 16 na chakula roho zetu zinachohitaji. Ni mifanano gani tunayoiona? Ni mafunzo gani ya kiroho Bwana angetaka kuwafundisha Waisraeli kwa kutuma mana katika njia Aliyofanya? (Ona Yohana 6:31–35, 48–58). Ungeweza pia kuonesha moja au zaidi ya video inayopatikana katika “Nyezo za Ziada.”

Kutoka 17:8–16

Tunabarikiwa tunapowaidhinisha viongozi wetu.

  • Maelezo ya Haruni na Hur wakishikilia juu mikono ya Musa yanaelezea kwa mfano umuhimu wa kuwaidhinisha wale walioitwa kutuongoza. Ungeweza kuwaomba washiriki wachache wa darasa kuigiza uzoefu wakati mshiriki mwingine akiusoma kwa sauti kubwa. Jinsi gani juhudi za Haruni na Hur kushikilia mikono ya Musa zinafanana na juhudi zetu za kuwaidhinisha viongozi wetu? Jinsi gani tunaonesha kwamba tunawaidhinisha viongozi wetu?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Unaweza kupokea maelekezo yaliyo ya binafsi.

Dada Michelle Craig alifundisha:

“Kama mfuasi mwaminifu wa [Mwokozi], unaweza kupokea msukumo binafsi na ufunuo, wenye kukubaliana na amri zake, ambao unastahili kwako. Mnazo misheni za kipekee na majukumu ya kipekee ya kutekeleza maishani na mtapewa mwongozo wa kipekee kuyatimiza.

Nefi, kaka wa Yaredi, na hata Musa wote walitakiwa kuvuka sehemu kubwa iliyokuwa na maji—na kila mmoja ilifanya hivyo kwa njia tofauti. Nefi alifanyia kazi ‘mbao kwa ufundi maalumu’ [1 Nefi 18:1]. Kaka wa Yaredi alijenga mashua ambazo zilikuwa “zimekazwa kama bakuli’ [ona Etheri 6:5–8]. Na Musa “alitembea juu ya nchi kavu katikati ya bahari.” [Kutoka 14:29].

“Kila mmoja wao alipokea mwongozo binafsi, uliowafaa wao, na kila mmoja alionesha uaminifu na kutenda. Mungu anawakumbuka wale wanaotii na, kwa maneno ya Nefi, “atatayarisha njia kwa ajili yetu [sisi ili] kutimiza kitu ambacho ameamuru.’ [1 Nefi 3:7] Tambua kwamba Nefi anasema, ‘njia ‘—sio ‘ile njia.”

“Je, sisi tunakosa au kupuuza utumishi binafsi kutoka kwa Bwana kwa sababu ametayarisha ‘njia” tofauti na ile tunayoitarajia? (“Uwezo wa Kiroho,” Liahona, Nov. 2019, 21).

Video

Katika video “Daily Bread: Pattern,” “Daily Bread: Experience,” na “Daily Bread: Change” (ChurchofJesusChrist.org),), Mzee D. Todd Christofferson alishiriki utambuzi kuhusu muujiza wa mana.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Watie moyo Wengine Kutoa Ushuhuda. Wengi wa wale unaowafundisha wana ushahidi binafsi wenye nguvu wa ukweli wa kushiriki. Waalike kushiriki shuhuda zao kwa kuwauliza maswali ya kawaida, kama vile, “Umebarikiwa vipi kwa kumfuata nabii?” (Ona pia Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 11.)

Chapisha